Rosemary Peter avishwa Taji la Redd’s Miss Nyamagana 2013,baada ya Mshindi wa Taji hilo Diana Amimo kudanganya Uraia na Umri wake. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, June 07, 2013

Rosemary Peter avishwa Taji la Redd’s Miss Nyamagana 2013,baada ya Mshindi wa Taji hilo Diana Amimo kudanganya Uraia na Umri wake.



Rosemary Peter.
Rosemary Peter, ni mshindi wa pili katika shindano la kumtafuta Redds Miss Nyamagana 2013, shindano lililofanyika tarehe 11/05/2013 katika ukumbi wa JB Belmont Hotel jijini Mwanza.


Alhamisi ya tarehe 06/06/2013, Rosemary Peter amevishwa taji la Redds Miss Nyamagana 2013, baada ya Diana Amimo aliyekuwa mshindi wa taji hilo kudaganya Uraia na umri wake katika shindano hilo.
 

Udanganyifu huo uligunduliwa na kuthibitishwa na idara ya uhamiaji mkoa wa Mwanza, baada ya maafisa wake kumshikilia na kumuhoji mrembo huyo, wiki moja mara baada ya shindano hilo.



Rosemary peter akipongezwa baada ya kuvishwa Taji la Redd’s Miss Nyamagana 2013,baada ya Mshindi wa Taji hilo Diana Amimo kudanganya Uraia na Umri wake.


Rosemary peter  hapa anavishwa Taji la Redd’s Miss Nyamagana 2013,baada ya Mshindi wa Taji hilo Diana Amimo kudanganya Uraia na Umri wake.


Rosemary peter mshindi  Taji la Redd’s Miss Nyamagana 2013,baada ya Mshindi wa Taji hilo Diana Amimo kudanganya Uraia na Umri wake.

Kwa Mujibu wa kanuni na vigezo vya mashindano ya urembo hapa nchini, kuwa Msichana lazima awe raia wa Tanzania na mwenye umri wa miaka 18 hadi 24, Kampuni ya Stoppers Entertainment, imeweza kumvua taji mrembo Diana Amimo na kumvisha mshindi wa Pili Rosemary Peter kuwa Redds Miss Nyamagana 2013/14.



Aidha Sindano la kumtafuta Mrembo wa mkoa wa Mwanza  linatarajiwa kufanyika June 14,2013 katika viwanja vya Yatch Club jijini Mwanza.




Warembo 18 kutoka wilaya mbalimbali za mkoa wa Mwanza wamejitokeza kushiriki shindano hilo la aina yake huku....Burudani inayosubiriwa kwa hamu kubwa ni Mh. Mbunge Joseph Mbilinyi maarufu kama sugu atakapo panda jukwaani kukumbushia enzi hizo...akishindikizwa na mkali mwingine wa Chege Chigunda kutoka TMK.



Warembo wote wanatarajiwa kuanza kabi rasmi Jumanne hii katika moja ya hoteli maarufu jijini humo.



Itakumbukwa mkoa wa Mwanza tayari ulishatoa Mrembo wa Tanzania, ambaye ni Nasreem Karim 2009 na Miriam Gerald 2010.




Pamoja na mchakato wa shindano la urembo kuendelea kwa hivi sasa nchini, macho na masikio yapo mkoani Mwanza, ambako kumekua kukileta changamoto na upinzani mkali wa warembo kila Mwaka.


Hawa ni Warimbwende wa Sindano la kumtafuta mrembo wa mkoa wa Mwanza, linatarajiwa kufanyika June 14,20132  katika viwanja vya Yatch Club jijini Mwanza.Sura  Hizi hapa..ni balaa!! katika mapozz ya kila aina..kazi kwenu....anza kuvote na wa ukweli!!








Hawa ni Warimbwende wa Sindano la kumtafuta mrembo wa mkoa wa Mwanza, linatarajiwa kufanyika June 14,20132  katika viwanja vya Yatch Club jijini Mwanza.Sura  Hizi hapa..ni balaa!! katika mapozz ya kila aina..kazi kwenu....anza kuvote na wa ukweli!!




Picha na : Mukhsin Mambo.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad