Picha 20 za Mkutano Mkuu wa Vilabu 16 hai Vya Salamu ( RK Salam Club's ) Leo Jun 12,2013 katika Ukumbi wa Radio Kwizera FM wilayani Ngara Mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, June 12, 2013

Picha 20 za Mkutano Mkuu wa Vilabu 16 hai Vya Salamu ( RK Salam Club's ) Leo Jun 12,2013 katika Ukumbi wa Radio Kwizera FM wilayani Ngara Mkoani Kagera.


Picha ya  pamoja ,Wafanyakazi wa Radio Kwizera na  Baadhi ya Viongozi wa Vilabu 16 vya Salam vilivyoorodheshwa Radio Kwizera leo(Juni 12,2013) 2013 katika Viwanja vya  Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.


Picha ya  pamoja ,Wafanyakazi wa Radio Kwizera na  Baadhi ya Viongozi wa Vilabu 16 vya Salam vilivyoorodheshwa Radio Kwizera leo(Juni 12,2013) 2013 katika Viwanja vya  Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.




Baadhi ya Viongozi wa Vilabu 16 vya Salam vilivyoorodheshwa Radio Kwizera leo(Juni 12,2013) 2013  wakiendelea na Mkutano wao ndani ya ukumbi wa  Radio Kwizera , wilayani  Ngara mkoani  Kagera.





Baadhi ya Viongozi wa Vilabu 16 vya Salam vilivyoorodheshwa Radio Kwizera  wakiwa live katika kipindi cha RK Salam Club ,ndani ya Studio za Radio Kwizera -Ngara leo(Juni 12,2013)  wakati walipokutana kufanya  Mkutano wao wa kuchagua Rais wa Vilabu  ndani ya ukumbi wa  Radio Kwizera , wilayani  Ngara mkoani  Kagera.


Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi wa Rais,Makamu wa Rais,Katibu Mkuu na Msaidizi wake,Mhasibu na Kamati ya Nidhamu,Seif Omary Upupu mwenye shati la Kaki akihesabu moja ya kura za kuchagua Viongozi wa Umoja wa Watuma Salam wa  Vilabu 16 vya Salam  uliofanyika  leo(Juni 12,2013) 2013 katika Ukumbi wa  Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.

Baadhi ya watangazaji wa  Radio Kwizera ,toka Kushoto ni Seif Omary Upupu(News Editor),Joyce Ngallawa(Production Officer) na  Boazy Zobanya wakifatilia Mkutano wa  Baadhi ya Viongozi wa Vilabu 16 vya Salam  uliofanyika leo(Juni 12,2013) 2013 katika Ukumbi wa Mikutano wa   Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.

Dotto Bahemu akichukua taarifa kuhusu wale waliochaguliwa kuwa Viongozi  wa Vilabu 16 vya Salam vya  Radio Kwizera leo(Juni 12,2013) 2013 katika Ukumbi wa  Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.

Joyce Ngallawa ambaye ni Production officer wa  Radio Kwizera  akifatilia kile kilichokuwa kinaendelea katika Mkutano Mkuu wa   Baadhi ya Viongozi wa Vilabu 16 vya Salam vya Radio Kwizera leo(Juni 12,2013) 2013 katika Ukumbi wa Mikutano wa   Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.

Joyce Ngallawa ambaye ni Production officer wa  Radio Kwizera  akitoa neno kwa Niaba ya Uongozi wa Radio Kwizera  katika Mkutano Mkuu wa   Baadhi ya Viongozi wa Vilabu 16 vya Salam vya Radio Kwizera leo(Juni 12,2013) 2013 katika Ukumbi wa Mikutano wa   Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.

Kaimu Fundi Mkuu wa Radio Kwizera Yohana Bita akichukua matukio muhimu katika  Mkutano Mkuu wa   Baadhi ya Viongozi wa Vilabu 16 vya Salam vya Radio Kwizera leo(Juni 12,2013) 2013 katika Ukumbi wa Mikutano wa   Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.



Picha Juu na Chini ,Kushoto ni Mmiliki wa blog ya Mwana wa Makonda,Mohamed Ramadhani Makonda na Papa Clemence Nyandindi kutoka Kibondo RK Salam Club katika Picha ya pamoja ndani ya Studio za  Radio Kwizera leo(Juni 12,2013) 2013  mjini Ngara mkoani  Kagera.

Hawa ndio Viongozi waliochaguliwa na Baadhi ya Viongozi kuungoza Vilabu  16 vya Salam vya Radio Kwizera leo(Juni 12,2013) 2013 katika Ukumbi wa Mikutano wa   Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.

  Baadhi ya Viongozi wa Vilabu 16 vya Salam vya Radio Kwizera wakiwa kwenye Mkutano wao Mkuu leo(Juni 12,2013) 2013 katika Ukumbi wa Mikutano wa   Radio Kwizera  mjini Ngara mkoani  Kagera.


Mkutano wa RK Salam Club's Jun 12,2013 katika Ukumbi wa RK mjini Ngara wakiwa hapa pamoja na Mengine wakichagua Rais wa RK Club,Katibu Mkuu na Mhasibu Mkuu ili kukuza Upendo,Amani,Ushirikiano na Maendeleo katika Jamii.




RK Salam Club's hizo  ni pamoja na Muungano RK Salam Club,Nterungwe RK  Salam Club,Wema RK Salam Club,Mwilamvya RK Salam Club,Laight  RK Salam Club Lulembela,Nyakisasa RK Salam Club,Biharamulo  RK Salam Club,Ushirikiano RK Salam Club,Uhuru RK Salam Club,Umoja RK Salam Club,Wazalendo RK Salam Club.




Uchaguzi huo wa Umoja wa Watuma Salamu wa Radio Kwizera (RK  Salam Club's) umehusu Wajumbe wake ambao ni Mwenyeviti,Katibu na Wahasibu wa Vilabu 16 Vilivyosajiliwa na Hai vya Radio kwizera kuchagua Uongozi wa Umoja huo kwa nafasi ya  Rais ,Makamu Rais,Katibu Mkuu na Katibu Msaidizi,Mhasibu Mkuu pamoja na Kamati ya Nidhamu.




Akitangaza motokeo  Katika Uchaguzi huo ,Mwenyekiti wa Uchaguzi  Seif Omary Upupu amesema Jumla ya wapiga kura walikuwa ni 34 na kumtangaza Rais aliyechaguliwa kuwa  ni Mwl.Joshua Kaijage kwa kupata kura 23 kutoka Mwilamvya RK salam CLub,akiwashinda wagombea wenzake Paskari Mbugani kura 8 na Clemence Nyandindi kura 3.




Makamu wa Rais wa Umoja wa Vilabu hivyo vya RK ni Kawese Andrea kutoka Nyakisasa RK salam Club kwa kura 13,akiwashinda Paschal Mbugani kura 11 na Clemence Nyandindi kura 10.




Katibu Mkuu wa Umoja huo wa Vilabu vya Salama Vya Radio Kwizera ni Yasin Gwamasunzu kutoka RK Laight Salam Club kwa kupata Kura 22 na kuwashinda wagombea wenzake Sinani Ngomambili kura 8,Erenest Kuguru kura 2 huku kura 2 zikiharibika.




Aidha katika Nafasi ya Katibu Msaidizi wa umoja huo,ametangazwa ni Paschal Mbugani aka Mzee wa Haba na Haba kutoka Wema RK Salam Club kwa kupata kura 21 na kuwashinda Juma Ayubu aliyepata kura 8 na Melkior Sheshahu kura 4 huku kura Moja ikiharibika.




Mwenyekiti wa Uchaguzi huo Seif Omary Upupu amemtangaza   Papa Clemence Nyandindi kuwa Mhasibu wa Umoja huo wa Salama Radio Kwizera kwa Kupata kura 23,akiwabwaga wapinzani wake Sixmundi Mgalula kura 7 na Kachumita Zefrini  kwa kupata kura 7 huku kura moja ikiharibika.




Katika mkutano huo Mkuu wa Vilabu vya Watuma Salam wa Radio Kwizera,ilichaguliwa Kamati ya nidhamu ya watu watano ambao ni pamoja na Richard Galila,Amon Zenobi,Sixmundi Mgalulua,Bandora Kakenguzi na Marindi wa Marindi.




Ikumbukwe kuwa Radio Kwizera iliona Umuhimu wa kuwa karibu na Vilabu hivyo vya Salam  ili kuwaleta watu pamoja, ili washirikiane kwa pamoja lengo likiwa ni kuleta Umoja,Upendo na Maendeleo katika Jamii.


Vilabu hivyo Vya Salam Vilivyosajiliwa Radio Kwizera  ambavyo ni hai ni pamoja na:-



:- Mwilamvya  RK  Salam Club ,wilayani Kasulu.


:- Umoja RK Salam Club,Mwanga Barabarani wilayni Biharamulo.


:- Light RK Salam Club,Lulembela wilayani Bukombe.


:- Amani RK Salam Club,Kalambi wilayani Muleba.


:- Muungano RK Salam Club,Muzani Nyakahura wilayani Biharamulo.


:- Camp la Waparanganaji RK Salam Club,Ushirombo.


:- Wema RK Salam Club,Ruganzo wilayani Biharamulo.


:- Kumwendo RK Salam Club,wilayani Ngara.


:- Ushirikiano RK Salam Club ,Katahoka wilayani Biharamulo.


:- Nterungwe RK Salam Club,Nterungwe wilayani Ngara.


:- Chapa Jembe RK Salam Club,Nyabusozi wilayani Biharamulo.


:- Biharamulo RK Salam Club,wilayani Biharamulo.


:- Wazalendo RK Salam Club,Kazilamyaye Runzewe.


:- Mauzo Basanza RK Salam Club,wilayani Uvinza Kigoma.


:- Kibondo RK Salam Club, wilayani Kibondo.


:- Nyakisasa RK Salam Club,wilayani Ngara.


Aidha Radio Kwizera FM ya Wilayani Ngara mkoani Kagera ni Mlezi wa Vikundi hivyo vya Salama na wanaunganishwa kupitia kipindi cha RK Salam Club  kila siku za Jumatano na Ijumaa kwa Lengo la kukuza Amani,Upendo,Ushirikiano na Maendeleo katika Jamii wanayoishi.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad