Mario Gomez apiga Bao mbili na kuifanya Bayern Munich kuweka Historia ya kuwa Klabu ya kwanza ya Ujerumani kuweza kushinda makombe Matatu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, June 02, 2013

Mario Gomez apiga Bao mbili na kuifanya Bayern Munich kuweka Historia ya kuwa Klabu ya kwanza ya Ujerumani kuweza kushinda makombe Matatu.



Jupp Heynckes
Winga  machachari wa klabu ya Bayern Munich, Franck Ribery ameonyesha furaha yake baada ya klabu yake kuifunga  VfB Stuttgart kwa mabao 3-2 katika fainali ya DFB-Pokal na kuweka historia ya kuwa klabu ya kwanza nchini Ujerumani kushinda mataji matatu kwa mkupuo. 




Winga huyo wa kimataifa wa Ufaransa amesema kuwa anajisikia furaha na mafanikio hayo ya kihistoria waliyopata ni kutokana na juhudi pamoja na malengo waliyojiwekea. 




Ribery aliwashukuru wachezaji wenzake pamoja na mashabiki ambao wamekuwa nao katika kipindi chote na kuahidi kuwa ataendelea kuwepo klabuni hapo kwa kipindi kirefu kijacho. 




Naye nahodha wa klabu hiyo Philipp Lahm aliongeza kuwa juhudi zao za ndani na nje ya uwanja ndizo zilizowafikisha hapo.




Bayern walifanikiwa kuweka kibindoni taji la Ligi Kuu ya Ujerumani mapema mwezi uliopita kabla  wiki moja baada ya kuifunga Borussia Dortmund katika Champions League  pale Wembley, waliingia kwenye fainali ya DFB Pokal wakijiamini vilivyo na  wakaongoza mchezo huo kwa mabao 3-0 kabla Stuttgart kufunga mabao mawili ndani ya dakika 10 za mwisho wa mchezo huo.




Hii hapa ndio listi ya vilabu vya UEFA ambavyo vimewahi kubeba makombe matatu ndani ya msimu mmoja (kombe la ligi, kombe la Fa, na Kombe la ulaya):-


Bayern Munich (Germany) 2012/2013.

Inter Milan (Italy) 2009/2010.

FC Barcelona (Spain) 2008/2009.

Manchester United (England) 1998/1999.

PSV Eindhoven (Netherlands) 1987/1988.

Ajax (Netherlands) 1971/1972.

Celtic (Scotland) 1966/1967.



Hiyo ilikuwa Mechi ya mwisho kwa Kocha wa Bayern Jupp Heynckes ambae anastaafu na nafasi yake kuchukuliwa na aliekuwa Kocha wa FC Barcelona Pep Guardiola.



Mbali ya Bao 2 za Mario Gomez, Bao la kwanza la Bayern lilifungwa na Penati ya Thomas Mueller.



Bao za Stuttgart zilifungwa na Martin Harnick.



Huu ni ushindi wa 15 katika Mechi 16 walizocheza mwisho Bayern Munich na kipigo chao cha mwisho walikipata Oktoba Mwaka jana.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad