Kutokana na kifo cha Msanii Albert Mangweha, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo yatoa Salama zake za rambi rambi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, June 02, 2013

Kutokana na kifo cha Msanii Albert Mangweha, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo yatoa Salama zake za rambi rambi.



Albert Mangweha.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, imepokea kwa mshituko na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo fleva) Albert Mangweha, aliyefariki huko Afrika  Kusini katika hospitali ya St. Hellen akiwa katika shughuli za muziki, Jumanne  tarehe 28 Mei, 2013.


Kifo cha Albert Mangweha ni pigo kubwa kwa fani ya muziki hapa nchini, na pia kimataifa. Na kutokana na umahiri wake katika fani hiyo ya muziki wa kizazi kipya hususan aina yake ya uimbaji ya “Free Style” alikonga mioyo ya wapenzi wake hasa vijana ndani na nje ya nchi.


Albert Mangweha atakumbukwa na wasanii na wapenzi wa muziki  kwa kipaji na juhudi zake za kukuza muziki hapa nchini.

Serikali inawapa pole ndugu na jamaa wote  na kuwaomba wawe na uvumilivu na subira katika kipindi cha msiba.



Wito wa Serikali kwa wasanii na wananchi kwa ujumla ni kuendelea kumuenzi kwa  yale yote mazuri aliyoyafanya wakati wa uhai wake.



Mwenyenzi Mungu ailaze roho ya Albert Mangweha mahala pema peponi.”




Imetolewa na

Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo

Dkt Fenella Mukangara.





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.


Kamati ya msiba tunaomba kutoa ya taarifa kwamba mwili wa Ndugu yetu Albert Mangweha hautoweza kufika siku ya Jumapili ya tarehe 2/06/2013 kama ilivyo taarifiwa hapo awali, hii ni kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu.



Kwa sasa tunasubiri taarifa kamili kutoka kwa wenzetu/wawakilishi wetu waliopo nchini Afrika Kusini, mara tutakapopata taarifa hizo tutawafahamisha zaidi.



Tunaomba radhi Watanzania wote kwa usumbufu wote uliojitokeza tushirikiane na uvumilivu kwa hili.


Asante

Mwenyekiti wa Kamati

Kenneth Mangweha.

 

Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Radhia Msuya, akiweka saini katika kitabu cha maombelezo nyumbani kwa baba mdogo wa Marehemu Mangweha Mbezi Beach jijini Dar leo.


Balozi Msuya akimpa mkono wa pole mama mdogo wa Marehemu Mangweha, Ella Mangweha.


Balozi Msuya (katikati) akibadilishana mawazo na baba mdogo wa marehemu David Mangweha (kulia) na mama mdogo Ella (kushoto).



Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Radhia Msuya amefika nyumbani kwa mama mdogo wa marehemu Mangwea Mbezi, Goige jijini Dar es Salaam, leo na kutoa neno.
 


Akizungumzia msiba wa Albert Mangwea alisema amesikitishwa sana na kama Mtanzania, amewapa pole ndugu, jamaa, marafiki na wanamuziki wote nchini.




Akizungumza katika msiba huo alisema: “Mtu anayefia hospitali na nyumbani ni tofauti, alitakiwa kufanyiwa uchunguzi, ubalozi unafanyia kazi kibali ambacho kinatarajiwa kupatikana kesho (Jumatatu), ili ikiwezekana mwili wa marehemu uwasili hapa nchini Jumanne.




Taratibu zinazopitiwa ni za kawaida ila kwa kutokana na umaarufu wa aliyefariki ndiyo inaonekana hivyo, hata kama ingetokea hapa kwa mtu wa nchi nyingine utaratibu ungekuwa ni uleule.



Nitoe wito kwa vijana kuwa wanapokuja Afrika Kusini wanatakiwa kufuata taratibu na kutoa taarifa ubalozini, hiyo inarahisisha kutoa msaada pindi kunapotokea tatizo,” alisema balozi Radhia.
 




Miraji Kikwete (kushoto) akikabidhi fulana kwa kwa ajili ya shughuli za msiba wa Mangweha. Katikati ni TID na P-Funk (kulia).


Miraji akiwa katika pozi na fulana sawa na ya marehemu Mangweha hapo chini.…


Marehemu Albert Kenneth Mangweha enzi za uhai wake.



Mdau wa muziki nchini, Miraji Kikwete ambaye ni mtoto wa Rais wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete leo amekabidhi fulana kwa ajili ya shughuli ya msiba wa msanii Albert Kenneth Mangweha katika Viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad