Inasemekana ,“Wananchi wengi wanapofanya ujenzi wa makazi yao hawathamini ujenzi wa vyoo bora ‘’. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, June 10, 2013

Inasemekana ,“Wananchi wengi wanapofanya ujenzi wa makazi yao hawathamini ujenzi wa vyoo bora ‘’.




Mganga mkuu mkoa wa Iringa, anasema licha ya takwimu kuonesha kuwa asilimia 62 ya watanzania wana vyoo bora hali halisi haiku hivyo kutokana na watu wengi kutothamini vyoo wakati wa ujenzi wa nyumba.




“Watu wanapofanya ujenzi wa makazi yao wanathamini na kutoa kipaumbele kwenye maeneo mengine ya nyumba na kuacha choo bila uangalifu mkubwa”,
Bw.Robert Salim  Mganga mkuu mkoa wa Iringa, anasema licha ya takwimu kuonesha kuwa asilimia 62 ya watanzania wana vyoo bora hali halisi haiku hivyo kutokana na watu wengi kutothamini vyoo wakati wa ujenzi wa nyumba.




Anasema wananchi wengi wanavyojenga nyumba zao hawatoi kipaumbele katika ujenzi wa vyoo bora jambo ambalo linaweza kuhatarisha afya zao na jamii kwa ujumla.




Watu wanapofanya ujenzi wa makazi yao wanathamini na kutoa kipaumbele kwenye maeneo mengine ya nyumba na kuacha choo bila uangalifu mkubwa”, alisema.




Anasema  hata shule nyingi za mijini na vijijini hazina matundu ya vyoo ya kutosha hivyo kusababisha huduma hiyo kuwa ya foleni.




Aliongeza kuwa katika shule moja yanatakiwa matundu ya vyoo 50 kwa wavulana na 40 kwa wasichana lakini hali ilivyo ni shule nyingi zimeruhusiwa kuendelea bila kukidhi vigezo.




Naye mwakilishi wa mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa, Donald Mshani anasema shule nyingi zimeruhusiwa kuendelea licha ya kukidhi vigezo kutokana na uchache wa rasilimali.




Naye Afisa afya wa mkoa wa Iringa, Didah Haruni anasema kwa takwimu zilizopo inaonesha kuwa kiwango cha uwepo wa vyoo ni kikubwa lakini bado kuna tatizo la muingiliano kati ya uchafu na binadamu. 




Chanzo: mjengwablog.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad