Hatimaye Redd's Miss Kigoma 2013 apatikana, ni Lilian Soti kutoka Mwanga mjini Kigoma. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, June 10, 2013

Hatimaye Redd's Miss Kigoma 2013 apatikana, ni Lilian Soti kutoka Mwanga mjini Kigoma.


Lilian Soti kutoka Mwanga mjini Kigoma Ni Redd's Miss Kigoma 2013,akiibuka Mshindi katika shindano liliofanyika Juni 09,2013 ndani ya ukumbi wa Kibo Peak.


Redd's Miss Kigoma 2013, kutoka kushoto ni mshindi namba 3 Happiness Albagost ,kati kati ni mshindi namba 1 Lilian Soti na kulia ni mshindi namba 2 Faidha Hamisi.


Top 5 ya Redd's Miss Kigoma 2013 ndani ya ukumbi wa Kibo Peak ikiwa ni  kati ya Warembo  12  walipambana jana(Juni 09,2013)  shindano kumtafuta Redd’s Miss Kigoma kwa mwaka huu 2013.



Emanuel J.Matinde na Waratibu wenzake wakifuatilia kwa makini moja ya matukio yaliyokuwa yakiendelea ndani ya ukumbi wa Kibo Peak kumtafuta Redd's Miss Kigoma 2013.



Wakionekana ni Warembo 12  ambao walipanda jukwaani (Juni 09,2013) katika Ukumbi wa Kibo Peak mjini hapa katika shindano kumtafuta Redd’s Miss Kigoma kwa mwaka huu.


Aidha Warembo  12  walipambana jana(Juni 09,2013)  katika Ukumbi wa Kibo Peak mjini Kigoma katika shindano kumtafuta Redd’s Miss Kigoma kwa mwaka huu 2013.




Kwa Mujibu wa Waratibu wa shindano hilo, mshindi wa kwanza wa mashindano hayo ameondoka na Printer kubwa yenye thamani ya shilingi laki 6 na fedha taslimu laki moja na nusu , sambamba na kushiriki shindano la kumtafuta mrembo wa Kanda ya Kati litakalofanyika mkoani Dodoma hivi karibuni.




Mshindi wa pili wa shindano la kumtafuta mrembo wa Mkoa wa Kigoma 2013, ameondoka na Printer yenye thamani ya shilingi laki 4 na fedha taslimu laki 1 na kushiriki shindano la Kanda ya Kati.




Mshindi wa tatu ameondoka na Microwave yenye thamani ya laki 2 na fedha taslimu elfu 70 pamoja na kushiriki shindano la kumatafuta mrembo wa Kanda ya Kati.




Picha na Habari Na:E.Johnson-Kigoma.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad