Wilaya ya Ngara na Ushindi wa Kishindo katika mashindano ya shule za sekondari nchini UMISETA ngazi ya mkoa wa Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, May 26, 2013

Wilaya ya Ngara na Ushindi wa Kishindo katika mashindano ya shule za sekondari nchini UMISETA ngazi ya mkoa wa Kagera.


Kikosi cha wachezaji 73  wa  michezo mbalimbali  kutoka Halmashauri ya wilaya ya Ngara katika mashindano ya shule za sekondari nchini UMISETA ngazi ya mkoa wa Kagera ,kimerejea salama  wilayani Ngara na ushindi mkubwa katika mashindano hayo  yaliyohitimishwa jana  katika viwanja vya chuo cha ualimu Katoke  mjini Muleba mkoani Kagera.



Timu ya UMISETA  2013 ya Manispaa ya Bukoba ikiingia uwanjani katika maandamano ya Pmaoja kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,tayari kushiriki Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).


Timu ya UMISETA  2013 ya Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ikiingia uwanjani katika maandamano ya Pmaoja kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,tayari kushiriki Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).


Timu ya UMISETA  2013 ya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara ikiingia uwanjani katika maandamano ya Pmaoja kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,tayari kushiriki Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).




Timu ya UMISETA  2013 ya Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi ikiingia uwanjani katika maandamano ya Pmaoja kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,tayari kushiriki Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).


Timu ya UMISETA  2013 ya Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo ikiingia uwanjani katika maandamano ya Pmaoja kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,tayari kushiriki Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).


Timu ya UMISETA  2013 ya Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe ikiingia uwanjani katika maandamano ya Pmaoja kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,tayari kushiriki Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).


Timu ya UMISETA  2013 ya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara ikiingia uwanjani katika maandamano ya Pmaoja kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,tayari kushiriki Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).



Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kagera ,Kanali Fabiani Masawe(Mulokozi) akiimba wimbo wa Kuhamasisha Maendeleo mkoa wa Kagera  wakati wa ufunguzi wa UMISETA  2013  kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,wa pili kushoto ni Afisa Elimu Mkoa wa Kagera Froliani Kimoro na Afisa Michezo mkoa wa Kagera Kefa Eliasi.



Afisa Michezo mkoa wa Kagera Kefa Elias akitenga mpira ili mgeni rasmi Kanal Fabiani Masawe afungue rasmi Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013)  kwenye Viwanja vya Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera.




Timu ya Mchezo wa Soka toka Wilaya ya Karagwe na Bukoba Vijijini wakielekea Jukwaa kuu kukaguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Fabiani Masawe ili kuanza kurusha karata zao katika mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013) kwenye uwanja wa soka wa chuo cha Ualimu Katoke.






Timu ya UMISETA  2013 ya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Katika mchezo wa Mpira wa pete(Netball) ikiwa Uwanjani  katika Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,tayari kushiriki Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).


 

Timu ya UMISETA  2013 ya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Katika mchezo wa Mpira wa pete(Netball) ikiwa Uwanjani  katika Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera ,tayari kushiriki Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).
Kikosi cha wachezaji 73  wa  michezo mbalimbali  kutoka Halmashauri ya wilaya ya Ngara katika mashindano ya shule za sekondari nchini UMISETA ngazi ya mkoa wa Kagera ,kimerejea salama  wilayani Ngara na ushindi mkubwa katika mashindano hayo  yaliyohitimishwa jana  katika viwanja vya chuo cha ualimu Katoke  mjini Muleba mkoani Kagera.




Akipokea msafara huo  leo(May 24,2013) katika Ukumbi wa halmashauri  ya wilaya ya Ngara ,mjini Ngara,kwa  niaba ya Mkuu wa wilaya ya Ngara Kostantine Kanyasu,Katibu tawala wa wilaya Tibaijuka Visent Josephati  amewapongeza mashujaa hao kwa kuipa ushindi wa kishindo  wilaya ya Ngara  katika UMISETA ngazi ya mkoa wa kagera na kuwataka wachezaji kuimarisha nidhamu na mazoezi ili  kujiendeleza zaidi kivipaji  vyao pamoja na kujitangaza kiajira.



Issa Sama ambaye ni  Mjumbe  wa  CCM - NEC Taifa na mdau mkubwa wa michezo hapa wilayani Ngara, licha ya kutoa usafiri wa kukisafikisha  kikosi hicho  kwa siku zote za mashindano ya UMISETA  ,amesema   kupata matunda yenye  mafanikio lazima viongozi kuwekeza nguvu zao kwa dhati na kushirikiana kwa pamoja  katika michezo ili  kuendeleza vipaji na kupata mafanikio kama hayo ambayo leo hii yameletwa ni wanafunzi  wa shule za sekondari  kupitia UMISETA ngazi ya mkoa wa Kagera.



Kwa Upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngara  Joni Shimilimana akizingumza katika mapokezi hayo  ndani ya viwanja vya Halmashauri ya wilaya ya Ngara ,amesema halmashauri hiyo itaendelea  kusaidia juhudi  za kuendeleza michezo  ili kuzidi kuitangaza wilaya ya Ngara kupitia sekta hiyo ya michezo.




Nae afisa elimu wilaya  ambaye kimashindano haya ya UMISETA ni Mwenyekiti   Juliasi  Nestori  amesema wilaya ya Ngara imetoa wachezaji 28 kati ya 108 wanaounda kikosi cha UMISETA  mkoa wa Kagera ambacho kimeanza kambi rasim leo  na kwamba wanaimani na wachezaji hao kufanya vema katika mashindano ya kikanda na  hata taifa pia.




Awali  Afisa Michezo wilaya ya Ngara  Said Salumu alitoa matokeo ya jumla  ya wilaya hiyo katika  mashindano hayo ya umiseta ngazi ya mkoa wa Kagera ambapo amesema Halimashauri ya wilaya ya Ngara katika mashindano ya UMISETA ngazi ya mkoa ilikuwa ni Jumla ya wilaya 7 zilizoshiriki katika mashindano hayo.




Amesema licha ya kupangwa kundi B lililokuwa ni timu za Wilaya za Bukoba Vijijini,Karagwe na Ngara  huku kundi A likiwa na Bukoba Manispaa,Biharamulo,Misenye na Muleba ,Wilaya ya Ngara ikaibuka Bingwa wa Kimkoa katika mchezo wa Mpira wa Kikapu kwa jumla ya Pointi 57  baada ya kuzifunga timu za Wilaya za Karagwe na Muleba na Kukabidhiwa Cheti cha Ushindi.




Katika mchezo wa Mpira wa Wavu(Volleyball),Said Salumu amesema wilaya ya Ngara ilicheza na Wilaya ya Bukoba na kuwafunga seti 2-0,Karagwe seti 2-0 na kuingia fainali na Wilaya ya Muleba na kufanikiwa kuwafunga seti 2-1 na hivyo kutangazwa Mabingwa wa mchezo huo Kimkoa.




Aidha kwenye Mchezo wa Pete(Netball) Wilaya ya Ngara ilizifunga timu za Wilaya ya Bukoba Vijijini na Karagwe na kuingia fainali dhidi ya wilaya ya Muleba na kufungwa magoli 19 – 9 na hivyo kuibuka washindi wa Pili Kimkoa.




Katika Mchezo wa Soka Mabingwa Kimkoa  walikuwa ni Wilaya ya Biharamulo ,wa pili Karagwe,tatu Kimkoa ni Ngara na wa nne Wilaya ya Misenyi huku Kipa bora kimkoa ni Nechi Mushi kutoka Wilaya ya Ngara.



Matokeo mengine katika Mbio za mita 1500,Mshindi wa pili kimkoa ni Sauli Semasanga kutoka Ngara,Mita 100 ni Dalali Mashughulu toka Ngara akiwa ni mshindi wa Kwanza Kimkoa.




Kuruka chini ,Mshindi wa Kwanza Kimkoa ni Maria Petter toka Ngara  huku Kuruka Juu akiwa ni mshindi wa Pili Kimkoa.



Pia Wilaya ya Ngara ikaibuka Bingwa Kimkoa katika Mchezo wa Hand ball.



Katika Mashindano hayo ya UMISETA mkoa wa Kagera wilaya ya Ngara imetoa wachezaji 28 na Walimu 3 kujumuika na Wachezaji wengine 108 kuunda kikosi cha UMISETA mkoa wa Kagera kitakachoenda kuunda Kikosi cha UMISETA kanda na Mkoa wa Kigoma ambapo  Mchezo wa Handball 9,Volleyball 4,Mpira wa Kikapu 3,Netball 3,Soka 3 na washindi Kimkoa katika Riadha na  Miluko.




Timu ya UMISETA  2013 ya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Katika mchezo wa Mpira wa Soka ikiwa Uwanjani  katika Chuo cha Ualimu Katoke wilayani Muleba mkoani Kagera , kutafuta nafasi ya kucheza Fainali dhidi ya Biharamulo ambapo ilifungwa bao 1 - o na hivyo kupata nafasi ya kuwania Mshindi wa tatu Kimkoa katika Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).






Anaepiga Makofi ni Nechi Mushi akichaguliwa kuwa Kipa bora katika ,kuunda Kikosi cha wachezaji 108 wa UMISETA mkoa wa Kagera katika  Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).


Afisa Michezo wilaya ya Ngara Said Salum akitoa taarifa ya Ushiriki ya wilaya hiyo katika  Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013) ndani ya Ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara ,ilipopokelewa kishujaa na Viongozi mbalimbali wa Kiserikali na Kisiasa (May 24,2013) pembeni yake ni Mwl.Baraka mratibu UMISETA wilaya.




Kuanzia Kushoto ni Afisa Elimu wilaya ya Ngara Julias Nestory, Issa Sama ambaye ni  Mjumbe  wa  CCM - NEC Taifa na mdau mkubwa wa michezo hapa wilayani Ngara , Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngara  Joni Shimilimana, Katibu tawala wa wilaya Tibaijuka Visent Josephati na Mwenyekiti wa Huduma za Jamii na Diwani wa Kata ya Mugoma Bw.Rubagola wakipokea taarifa ya ushiriki wa Wilaya ya Ngara katika Mashindano ya UMISETA Mkoa wa Kagera (May 21 hadi May 23,2013).




Katibu tawala wa wilaya Tibaijuka Visent Josephati  amewapongeza mashujaa hao kwa kuipa ushindi wa kishindo  wilaya ya Ngara  katika UMISETA ngazi ya mkoa wa kagera na kuwataka wachezaji kuimarisha nidhamu na mazoezi ili  kujiendeleza zaidi kivipaji  vyao pamoja na kujitangaza kiajira.


Kwa Upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngara  Joni Shimilimana akizingumza katika mapokezi hayo  ndani ya viwanja vya Halmashauri ya wilaya ya Ngara ,amesema halmashauri hiyo itaendelea  kusaidia juhudi  za kuendeleza michezo  ili kuzidi kuitangaza wilaya ya Ngara kupitia sekta hiyo ya michezo.


Afisa Elimu wilaya ya Ngara Julias Nestory, amesema wilaya ya Ngara imetoa wachezaji 28 kati ya 108 wanaounda kikosi cha UMISETA  mkoa wa Kagera ambacho kimeanza kambi rasim leo  na kwamba wanaimani na wachezaji hao kufanya vema katika mashindano ya kikanda na  hata taifa pia.


Issa Sama ambaye ni  Mjumbe  wa  CCM - NEC Taifa na mdau mkubwa wa michezo hapa wilayani Ngaraamesema   kupata matunda yenye  mafanikio lazima viongozi kuwekeza nguvu zao kwa dhati na kushirikiana kwa pamoja  katika michezo ili  kuendeleza vipaji na kupata mafanikio




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad