![]() |
Wachezaji wa
Buyern Munich wakishangilia Ubingwa wa UEFA Champions League 2012/2013 na kuwa Washindi
wa Kombe hili kwa mara ya 5.
|
![]() |
Arjen Robben
received Man of the Match award from Sir Alex Ferguson.
|
![]() |
Jürgen Klopp
consoles his BVB players after their UEFA Champions League final defeat.
|
![]() |
Ilkay
Gundogan wa Borussia Dortmund akiifungia timu yake bao la kusawazisha kwa
penalti dakika ya 67 ya mchezo.
|
![]() |
Mario
Mandzukic (9) wa Buyern Munich akiifungia timu yake bao la kuongoza dakika ya
60 ya mchezo huo wa fainali.
|
![]() |
Wachezaji wa
Buyern Munich wakishangilia bao lao la pili na la ushindi lililofungwa na Arjen
Roben dakika ya 89 ya mchezo.
|
Goli la dakika
ya 89 la
Mchezaji toka Uholanzi Arjen Robben limefuta gundu kwake na Klabu yake ya Bayern Munich ya Ujerumani katika Fainali za
UEFA Champions League, baada ya Bao hilo kuipa ushindi wa magoli 2-1
Bayern dhidi ya wenzao wa Ujerumani
Borussia Dortmund katika Mechi iliyochezwa Uwanja Wembley Stadium Jijini
London nchini Uingereza hapo Jumamosi (May 25,2013)Usiku.
![]() |
Arjen Robben
|
Bayern
walipoteza Fainali mbili za Champions League katika Miaka mitatu iliyopita,
ikiwemo kutolewa kwa Mikwaju ya Penati na Chelsea Mwaka jana tena katika Uwanja
wao wenyewe Allianz Arena lakini safari
hii waliibuka Washindi wa Kombe hili kwa mara ya 5.
Ni Real
Madrid toka Hispania ni Bingwa wa
Champions League mara 9 na AC Milan ya Italia akiwa ni Bingwa wa
Champions League mara 7, ndio wameshinda Kombe hili mara nyingi kupita Bayern
Munich.
Mabingwa
wengine wa UEFA Champions League ni Liverpool ya Uingereza mara 5, FC Barcelona ya Hispania Mara 4, Ajax ya
Uholanzi Mara 4, Inter Milan ya Italia
mara 3 na Manchester United ya Uingereza mara 3.
![]() |
Jupp Heynckes |
Kwa Kocha
wao, Jupp Heynckes, huu ni ushindi mtamu kwa vile anastaafu na nafasi yake
kuchukuliwa na aliekuwa Kocha wa FC Barcelona, Pep Guardiola kwa ajili ya Msimu
ujao.
Mara baada
ya Filimbi ya mwisho kulia, Arjen Robben alitokwa machozi kwani alikuwepo
wakati Bayern Munich inapoteza Fainali mbili kwa Inter Milan, Mwaka 2010, na
Chelsea, 2012, ambapo alikosa Penati katika Mikwaju ya Penati iliyoipa Chelsea
Ubingwa, na vile vile akiwa na Chelsea katika Miaka ya 2005 na 2007 walitolewa
kwenye Nusu Fainali ya Mashindano haya na mara zote hizo walikuwa ni Liverpool
ndio waliowabwaga.
Mechi hii
ilitangaza vyema Soka la Kushambulia la Ujerumani kwani magoli ya Bayern Munich
yalifungwa na Mandzukic Dakika ya 60 na Robben dakika ya 89 huku
goli la Borussia Dortmund likifungwa na Mandzukic Dakika ya 68 kwa Mkwaju wa Penati.
No comments:
Post a Comment