Matokeo ya
mtihani wa kidato cha sita yaliyotarajiwa kutangazwa mwezi huu yatachelewa ili kutoa nafasi kwa Baraza la Mitihani la
Taifa (Necta), kurekebisha matokeo
mabaya ya mitihani kidato cha nne ya
mwaka jana yaliyofutwa na serikali mwezi
huu.
Matokeo ya
kidato cha sita ambayo huwa yanatangazwa mwanzoni mwa mwezi Mei mpaka sasa hayajatolewa na kwamba hayatatangazwa mpaka matokeo mapya
ya kidato cha nne yatakaporekebishwa rasmi.
Alipoulizwa juu ya suala hilo, Naibu Waziri wa Elimu na
Mfunzo ya Ufundi Philipo Mulugo
alisema ingawa wakati huu ndio unaopaswa yatangazwe matokeo ya kidato cha sita
haitafanyika hivyo hadi yatangazwe matokeo mapya ya kidato cha nne baada ya
kufutwa.
Hata hivyo,
akasema huenda yakatolewa pamoja au
yakafuata wakati mwingine lakini mara baada ya
kukamilisha kazi ya kurejea na kusahihisha matokeo ya kidato cha nne.
![]() |
Philipo Mulugo. |
"Siyo
kwamba yamechelewa kwani muda wa kujiunga na chuo ni Septemba hivyo
haitawaathiri kwa hilo," alisema Mulugo.
Kuhusu hatma
ya wanafunzi wa kidato cha nne ambao wapo mashuleni wanaendelea na masomo ya
kidato cha sita, alisema kama kutakuwa
na wanafunzi ambao wapo madarasani shule
zilizowasajili zitakuwa hazijafuata
mfumo wa elimu unavyoelekeza.
Alifafanua
kuwa mfumo wa elimu kwa kidato cha nne ulibadilishwa na kwamba endapo
mwanafunzi akifaulu anatakiwa kujiunga rasmi kidato cha sita Julai na si vinginevyo.
Alisema
licha ya ucheleweshaji wa matokeo
hali hiyo haikuwaathiri wanafunzi hao kwa kuwa ratiba ya kwenda masomoni haijaanza kwa mujibu wa kalenda ya shule ya serikali.
![]() |
Bungeni mjini Dodoma. |
Wiki
iliyopita serikali ilichukua uamuzi mgumu na kufuta matokeo kidato cha nne ya
mwaka 2012.
Uamuzi huo
mgumu ulifanywa na Baraza la Mawaziri kabla ya tume ya Waziri Mkuu kuwasilisha
ripoti yake kama njia ya kuwafariji wanafunzi waliofeli mtihani na kulitaka
Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) kuyapanga upya kwa kutumia utaratibu wa
kupanga madaraja uliotumika mwaka 2011.
Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi,
akiwasilisha kauli ya serikali bungeni mjini Dodoma Ijumaa iliyopita, alisema
utaratibu mpya uliotumika kupanga madaraja ulichangia katika matokeo mabaya
yaliyosababisha zaidi ya asilimia 60 ya wanafunzi kupata sifuri.
Februari
mwaka huu, Dk. Kawambwa alitangaza matokeo ya kidato cha nne na kubainisha kuwa
watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 walipata sifuri, huku wanafunzi 23,520
tu ambao ni sawa na asilimia 5.16 ndiyo waliofaulu na wengine 103,327 sawa na
asilimia 26.02 walipata daraja la nne.
Watahiniwa
walikuwa 456,137 kati yao wa shule wakiwa 397,136 huku wa kujitegemea 68,806.
Kwa mujibu
wa matokeo hayo, watahiniwa waliopata daraja la kwanza ni 1,641, wavulana
wakiwa 1,073 na wasichana 568, daraja la pili ni 6,453, wavulana wakiwa 4,456
na wasichana 1,997.
Matokeo hayo
yaliibua mjadala mkali huku makundi mbalimbali ya jamii yakihoji sababu
zilizosababisha wanafunzi wengi kufeli na kutaka Kawambwa na wasaidizi wake
wawajibike kabla Waziri Mkuu kuunda tume iliyoongozwa na Profesa Sifuni Mchome
kuchunguza ili kupata ufumbuzi wa kudumu.
No comments:
Post a Comment