Viongozi wa bara Afrika wanasherehekea miaka 50 tangu kuundwa kwa Umoja wa Afrika. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, May 26, 2013

Viongozi wa bara Afrika wanasherehekea miaka 50 tangu kuundwa kwa Umoja wa Afrika.




Muono wa jicho la samaki katika Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013.



Viongoi mbali mbali wa nchi za Umoja wa Afrika (AU) wakiwakumbuka waliotangulia mbele ya haki.





Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013. 



Marais Wastaafu wakiwa katika Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013.PICHA NA IKULU.



Viongozi wa bara Afrika wanasherehekea miaka 50 tangu kuundwa kwake hapo tarehe 25 Mei 1963 kwa jina la Umoja wa Nchi Huru za Afrika kuongoza mapambano dhidi ya ukoloni na kumaliza utawala wa ubaguzi wa rangi nchini Afrika ya Kusini. 




Sherehe za maadhimisho hayo zinafanyika leo(May 25,2013) mjini Addis Ababa  nchini Ethopia.




Mwenyekiti wa Umoja huo Waziri Mkuu wa Ethopia Hailemariam Desalegn katika hotuba ya ufunguzi, amesema sherehe hizo zitatafuta kuwepo kwa bara lisilokuwa na umaskini na mizozo na Afrika ambayo raia wake wanafurahia hadhi ya kipato cha kadri.




Umoja wa Afrika (AU)  wa nchi wanachama 54 ulichukua nafasi ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) uliyoanzishwa mwaka 1963  katika harakati za mataifa mengi kujinyakulia uhuru.




Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban ki Moon,Rais wa Brazil Dilma Rouseff na waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry ni miongoni mwa viongozi wa kimataifa waliojumuika na viongozi wa Afrika kusherehekea miaka 50 ya Umoja wa Afrika.




Rais wa Ufaransa Franswaa Hollande na makamu Waziri Mkuu wa China Wang Yang pia wanatarajiwa kuhudhuria sherehe hizo.




Makundi mbali mbali ya densi yatawatumbuiza wageni waalikwa wapatao 10,000 katika mji huo mkuu wa Ethopia.




Umoja wa Afrika unatimiza miaka 50 Tokea mabadiliko ya kidemokrasia katika Rasi ya Matumaini Mema na kumalizika vita baridi, Umoja huo unatafuta njia za kuwa na msimamo wake wenyewe.




Unalenga kuleta ushirikiano wa kikanda, kuondoa vizuizi vya lugha na biashara na hatimaye siku moja kuleta muungano wa bara zima la Afrika.




Miaka sita kabla ya hapo, muasisi Nkurumah kutoka kile kilichokuwa kikijulikana kama koloni la Uingereza "Pwani ya Dhahabu", leo hii Ghana, aliiongoza nchi hiyo kuwa huru na akawa ndiye baba wa vuguvugu la uzalendo wa Mwafrika katika kuliongoza jukwaa la mataifa machanga kupambana dhidi ya ukoloni na ubaguzi wa rangi.




Muongozo muhimu, ambao ni ule wa kutoingilia mambo ya ndani ya mataifa mengine huru, ukageuka hatimae kuwa janga kwa Umoja huo, kwani mtindo wa mapinduzi ya kijseshi wa miaka ya 1960 na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilipotokea, viongozi wa mataiafa ya Afrika walibakaia kimya wakiangalia .




Baada ya kuupa jina jipya la Umoja wa Afrika (AU) ambao uliundwa 2002 mjini Durban, Afrika ya Kusini, baada ya kumalizika vita baridi, madhumuni yake yakawa ni kuleta muungano wa kiuchumi na demokrasaia.




Kiroja cha mambo katikati ya miaka ya 1990, kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi aliyejitangaza "Mfalme wa Wafalme" wa Afrika, alilazimisha fikra ya mtazamo wa Nkrumah wa "Muungano wa Afrika,", ingawa ilikuwa siasa kwa masilahi ya kisiasa ya Gaddafi kuliko kuwa hatua ya kifalsafa.




Hata hivyo, mpango wake wa kuwa na jeshi moja, sarafu moja, biashara na kusafiri bila vizuizi kama ilivyo katika Umoja wa Ulaya ulisababisha mgawanyiko zaidi kuliko umoja. 




Kutokana na mvutano huo kukazuka kambi mbili na Afrika ya Kusini yenye nguvu kisiasa ikasimama kumpinga Gaddafi.




"Bila shaka matokeo kwetu si ya kuridhisha. lakini tunasonga mbele pamoja na nina hakika siku hadi siku tutafikia karibu lengo la "Muungano wa Afrika."




Alisema mjumbe wa Gaddafi kwenye Umoja huo, baada ya kuvunjwa moyo na kile alichokiona ni udhaifu, aliwaambia wajumbe baada ya kuchaguliwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika 2009.




Hayati  Gaddafi mara kwa mara alikuwa akitowa matamshi makali kwa waliompinga kwa kuzingatia kile alichokiona ni mapenzi ya Waafrika wengi kwake.




Hatimaye Ingawa wazo hilo lilizusha mabishano na kutoa sura ya mgawanyiko miongoni mwa mataifa, Umoja wa Afrika sasa una waziri wa ndani wa Afrika ya Kusini Nkosazana Dlamini-Zuma kama Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja huo, mwana mageuzi aliyetangaza haraka kwamba anataka kuona unawajibika zaidi.




Halmashauri hiyo kuu inataka kuendeleza sera ya kuadhibu kwa kusimamisha uanachama na vikwazo kwa wanaokiuka katiba na muongozo wake.




Mtihani kwa uwajibikaji na nguvu za kiutendaji za Umoja wa Afrika, kandoni mwa pigo la ujumbe wake wa AMISOM nchini Somalia, ni mgogoro katika mataifa ya Afrika ya Magharibi ya Mali na Jamhuri ya Afrika ya Kati.




Kwa Maoni "Leo Afrika ni ya kidemokrasia zaidi kuliko miaka kumi iliyopita ambapo tulikuwa na serikali chache zilizochaguliwa kidemokrasia. 




Lakini hili halipaswi kutafsiriwa kwamba ni uongozi wa kidemokrasi. 




Demokrasia ni kutambua fikra tafauti, kwani ndiyo msingi wa matatizo ya kisiasa Afrika."


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad