Mtwara :Ni vema tuache sauti ya wananchi kusikika na kuzitolea maamuzi sahihi yenye kujenga kuaminiana na kuheshimiana kati ya dola na wananchi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, May 25, 2013

Mtwara :Ni vema tuache sauti ya wananchi kusikika na kuzitolea maamuzi sahihi yenye kujenga kuaminiana na kuheshimiana kati ya dola na wananchi.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Dkt.  Emmanuel  Nchimbi  akitoa kauli ya Serikali Bungeni kuhusu vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara.



Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda  akiahirisha Bunge kutokana na vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara.


Waziri wa Nchi  ofis ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)  Merry Nagu akiomba kutengua kanuni  ya Bunge  Na. 38 ili kuruhusu suala la vurugu za Mtwara kujadiliwa Bungeni.


Waziri Mkuu Mhe.  Mizengo Pinda akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Frederick Werema  pamoja na baadhi ya Mawaziri   ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirishwa kwa kikao cha Bunge .


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Emmanuel Nchimbi (Kushoto) akizungumza na mbunge wa Kinondoni Mhe. Iddi Azzan nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya bunge kuahirishwa.



Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Prof. Sospeter Muhongo  akizungumza na baadhi ya Mawaziri na Wabunge ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha bunge


Wabunge wa Viti Maalumu wakiwa nje ya ukumbi wa Bunge baada ya Spika kuahirisha Bunge. Kutoka kushoto ni Mhe. Lucy Owenya(CHADEMA), Katikati  Mhe. Mkiwa Kimwanga(CUF) na kulia ni Mhe. Dkt. Merry Mwanjelwa(CCM).


Naibu Waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi Pereira Ame Silima (Katikati), Naibu wa Viwanda na Biashara Mhe. Greygory Teu (kushoto) na mbunge wa Kilosa Mhe. Mustafa Mkullo wakizungumza nje ya ukumbi wa  Bunge.


Kundi la Waandishi wa Habari wanaoripoti  habari za Bunge wakitoka ndani ya ukumbi huo mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha kikao cha Bunge.PICHA NA ZAWADI MSALLA-MAELEZO DODOMA

Moja ya bango lenye ujumbe "Gesi ibaki au tugawane nchi" picha hii ni ya maktaba iliyopiwa katika vurugu hivi karibuni juu ya upingaji wa gesi kutoka Msimbati kwenda Dar es Salaam.


Wakati  Serikali ikiendelea kuwatupia wanasiasa lawama kuhusiana na vurugu za wakazi wa Mtwara wanaopinga hatua ya Rais Kikwete na Serikali kusafirisha Gesi hadi jijini Dar es Salaam kwa njia ya mabomba, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk Willbroad Slaa, amesema kwamba machafuko yanayotokea katika mkoa huo hayasababishwi na mambo ya kisiasa isipokuwa ni umaskini unaoikabili nchi.


Dk Slaa alisema kwamba umaskini huo unaosababisha vurugu za Mtwara zimesababishwa na CCM tangu zama za kale na si kwa siasa za sasa.
 



Alisema kwamba Wananchi hao  wameamua kufanya yote hayo kwa kuangalia wenzao wa mikoa mingine iliyojaliwa kuwa na mali nyingi katika mikoa yao na bado haiwanufaishi matokeo yake inakuwa ni mali yakuwanufaisha wengine bila wao kupata faida yoyote ile.




Katika hatua nyingine Dk Slaa alisema kwamba Serikali isikimbilie kulaumu wanasiasa bali itambue kwamba,siasa chafu zinafanya kazi kama watu ni masikini, lakini kama nchi itakuwa tajiri siasa chafu haziwezi kuwepo.



Mkazi wa Mtwaa akiwa anatimua mbio huku akiwa na mtoto baada ya kupigwa kwa bomu la machozi, kazi kweli kweli.


Nyumba ikiwa imebomolewa  baada ya kuchomwa moto.


Gari likiteketea kwa moto


Barabara ikiwa imewekwa vizuriwizi wakati wa vurugu hizo na kusababisha huduma mbalimbali za kijamii kudorola siku ya Mei 22/ 2013.



Serikali iangalie upya namna inavyolitazama suala la Mtwara. Hivi sasa suala hili linaonekana kiusalama zaidi badala ya kuliona kama suala la kijamii na maendeleo lenye kuhitaji kujenga imani ya wananchi. 




Suala hili linahitaji muda na heshima kwa wananchi. Ni vema tuache sauti ya wananchi kusikika na kuzitolea maamuzi sahihi yenye kujenga kuaminiana na kuheshimiana kati ya dola na wananchi.




Zitto Zuberi Kabwe
Suala la Mtwara ni zaidi ya gesi asilia. Ni matokeo ya kutengwa kimaendeleo kwa muda mrefu. Suala la Gesi ni nafasi ya kuunganisha watu wa kusini na Jamhuri ya Muungano. Tuamue sasa kufanya maamuzi sahihi na kuunganisha Jamhuri yetu au kukosea na kudharau na kuivunja Jamhuri yetu.




Kama Kuna mataifa ya kigeni/makampuni binafsi yanahusika na hali ya Mtwara. Serikali iyataje mataifa hayo na makampuni hayo hadharani na vibaraka wao.Vinginevyo nadharia hizi zitaonekana ni ni propaganda tu kwa lengo la kufunika kombe mwanaharamu apite. 




Nadharia zote za kuelezea masuala ya Mtwara zinakimbia suala la msingi ie kutengwa kwa muda mrefu sana kwa mikoa ya kusini kwenye maendeleo ya nchi. 


Ahadi za Rais Ben Mkapa kuhusu Mtwara Corridor, ahadi za Rais Jakaya Kikwete za 2005 na biashara ya korosho ni miongoni mwa malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wa Mtwara. Suala hili la msingi lazima lipatiwe majawabu mwafaka kwa maelezo yenye heshima kwa wananchi badala ya dharau na vijembe dhidi ya raia.




Kuna kukosa imani kukubwa kwa wananchi dhidi ya Serikali. Suala hili ni pana zaidi na linasambaa Tanzania nzima. Malalamiko yanaposhawishiwa kihofu tu huleta matatizo makubwa sana. Hali ya namna hii haijawahi kutokea nchini mwetu. Kukamata na kufunga viongozi wa wananchi haitosaidia kamwe. 




Kutumia nguvu ya dola kuzima vuguvugu la wananchi sio njia pekee ya kujenga amani. Makovu ya kutumia nguvu ya dola huchukua muda mrefu sana kupona. Lazima kubadili mkakati wa kuongoza na kuliweka Taifa sawa.




Zitto Zuberi Kabwe (Mb)

24th May 2013



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad