RAHA YA UBINGWA: FC Barcelona na Taji la 22 la Ligi Kuu Hispania, David Beckham na rekodi ya kutwaa Mataji ya Ligi Kuu na klabu za nchi nne tofauti. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, May 13, 2013

RAHA YA UBINGWA: FC Barcelona na Taji la 22 la Ligi Kuu Hispania, David Beckham na rekodi ya kutwaa Mataji ya Ligi Kuu na klabu za nchi nne tofauti.


HISPANIA : Lionel Messi alishindwa kucheza jana(May 12.2013) kutokana na kusumbuliwa na maumivu, lakini haikuzuia FC Barcelona kushinda 2-1 dhidi ya Atletico Madrid usiku wa jana na kushangilia taji la 22 la Ligi Kuu Hispania na wakiivua rasmi ubingwa Real Madrid. 


Mabingwa: Wachezaji wa Barcelona wakishangilia taji la La Liga.


Wachezaji  Atletico Madrid wakiwapa heshima yao wachezaji wa Barcelona kwa kuwa Mabingwa wa La Liga.



Atletico itamenyana na Real Madrid katika fainali ya Kombe la Mfalme Ijumaa(May17,2013).

Barcelona inaweza kufikisha rekodi ya Madrid msimu uliopita kufikisha pointi 100 kama itashinda mechi zake tatu zilizobaki.


Raha ya Ubingwa: David Beckham na Zlatan Ibrahimovic wakishangilia kuiwezesha PSG kutwaa taji la kwanza baada ya miaka 19.



UFARANSA: David Beckham ameweka rekodi ya kutwaa mataji ya Ligi Kuu na klabu za nchi nne tofauti, baada ya PSG kuifunga Lyon 1-0 na kutwaa ubingwa wa Ligue 1, Ufaransa.



Beckham, ambaye sasa anakuwa mchezaji wa kwanza wa Uingereza kutwaa mataji katika nchi nne tofauti, aliingia akitokea benchi, wakati Jeremy Menez alipokifungia bao pekee la ushindi kikosi cha Carlo Ancelotti.




Ubingwa wa PSG hautathibitishwa hadi Kamati ya Nidhamu ya Ligi itakapokutana kuamua kuipokonya pointi au la kufuatia tuhuma za Mkurugenzi wake, Leonardo kumrubuni refa.


Beckham akikumbatiana na mmiliki wa Qatari TV, chaneli ya Al Jazeera Sport ambaye pia ni mmiliki wa PSG, Nasser Al-Khelaif.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad