Kuelekea Fainali ya Champions League Uwanja wa Wembley kati ya Borussia Dortmund na Bayern Munich(May 25,2013) UEFA huenda ikangaza Bingwa wa Europa League kuingizwa moja kwa moja kucheza Champions League kuanzia Mwaka 2016. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, May 25, 2013

Kuelekea Fainali ya Champions League Uwanja wa Wembley kati ya Borussia Dortmund na Bayern Munich(May 25,2013) UEFA huenda ikangaza Bingwa wa Europa League kuingizwa moja kwa moja kucheza Champions League kuanzia Mwaka 2016.


Borrusia Dortmund wakiwasili Jijini London mapema leo(May 24,2013).



Roberto Lewandoski na wenzie ndani ya Heathrow Airport Jijini London mapema leo(May 24,2013).


Mario Gomez akiwasili Jijini London mapema leo(May 24,2013) in the Champions League final kati ya Bayern Munich  dhidi ya  Borussia Dortmund hapo kesho (May 25,2013).


Jurgen Klopp kocha wa Borrusia Dortmund ndani ya Heathrow Airport Jijini London mapema leo(May 24,2013) in the Champions League final..


Frank Ribery akilakiwa na umati wa mashabiki Jijini London mapema leo(May 24,2013) in the final kati ya Bayern Munich  dhidi ya  Borussia Dortmund hapo kesho (May 25,2013).


Ijumaa(May 24,2013)  UEFA imetangaza kuwa Bingwa wa Mashindano ya Europa League  atazawadiwa kwa kuingizwa moja kwa moja kucheza Mashindano makubwa ya Champions League kuanzia Mwaka 2016 ili    kuboresha Europa League na kuifanya ionekane muhimu.




Hatua hii inalenga kuifanya michuano ya Europa League ionekane ni muhimu badala ya kupondwa na kuonekana ni ngazi ya chini ya Champions League.




Uamuzi huu umefikiwa baada ya Majadiliano ya muda mrefu kati ya European Club Association (ECA), Chama cha Klabu Ulaya  na UEFA.




Mabingwa wa Europa  League.





-2013: Chelsea



-2012: Atletico Madrid



-2011: FC Porto



-2010: Atletico Madrid



-2009: Shakhtar Donetsk




- Europa  League huingiza Mapato kidogo na huwa na msisimko mdogo ukilinganisha na Champions League.




-Timu zinazomaliza Nafasi za 3 kwenye Makundi ya Champions League hutupwa kucheza Europa  League.




-Katika Fainali ya Mwaka huu ya Europa  League iliyokutanisha Timu zilizobwagwa kutoka Champions League, Chelsea iliifunga Benfica Bao 2-1 huko Amsterdam ArenA, Uholanzi Wiki iliyopita.







Wakati huo huo, UEFA imetangaza kuwa Mwaka 2015 Uwanja wa Olimpiki wa Berlin huko Germany ndio utachezwa Fainali ya Champions League na ule wa Mjini Warsaw huko Poland, wa National Stadium, ndio utachezwa Fainali ya Europa  League.




Bayern Munich coach Jupp Heynckes
Mipango mingine ambayo inajadiliwa na UEFA ambayo itakuwa na Mkutano wa Kongresi yake hapo Ijumaa Mjini London ikiwa ni Siku moja tu kabla Fainali ya Champions League kuchezwa Uwanja wa Wembley Jijini humo kati ya Borussia Dortmund na Bayern Munich, ni pamoja na kuziongezea Ligi kubwa za Ulaya nafasi za uwakilishi kwenye Champions League kuwa 5 badala ya 4 na kuongeza nafasi za kucheza Europa  League.




Pia, UEFA inataka kuondoa ule mtindo wa Timu zikiwa Mabingwa wa Champions League na Europa  League lakini hazikumaliza Ligi zao zikiwa zimefuzu kucheza Ulaya wao kucheza Ulaya badala ya zile Timu zilizomaliza Ligi Nafasi za juu na badala yake kuzibakisha Timu za juu kwenye Ligi kucheza Ulaya na Mabingwa Watetezi kuingia kutetea Mataji yao.




Uamuzi huu utaondoa hali iliyowakuta Tottenham Msimu wa Mwaka 2011/12 kwani walimaliza BPL, Barclays Premier League, wakiwa Nafasi ya 4 na Chelsea kumaliza Nafasi ya 6 lakini Nafasi yao kucheza Champions League ikachukuliwa na Chelsea kwa vile walitwaa Ubingwa wa Champions League na Tottenham kutupwa Europa  League.




Sheria zote hizi mpya zinatarajiwa kupitishwa Ijumaa huko London UEFA Kongresi itakapoketi na kuanza kutumika Mwaka 2016.




Pia UEFA imepitisha Adhabu kwa Kosa la Ubaguzi kuwa Kifungo cha Mechi 10 au zaidi, kumtukana Mwamuzi kutoka Mechi 2 hadi 3 au zaidi na kumshambulia Mwamuzi si chini ya Mechi 15 badala ya 10.




Sheria hizi mpya za Adhabu zitaanza Juni 1.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad