'Dawa za kuongeza nguvuza kiume sasa tishio Visiwani Zanzibar. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, April 19, 2013

'Dawa za kuongeza nguvuza kiume sasa tishio Visiwani Zanzibar.




Waziri wa Afya Zanzibar,

 Juma Duni Haji.
Waziri wa Afya Zanzibar, Juma Duni Haji, ameshangazwa na wimbi la uuzaji wa dawa za nguvu za kiume uliojitokeza katika maeneo ya misikiti visiwani humo.




Akifunga mjadala kuhusu ripoti ya Kamati ya Maendelo na Ustawi wa Jamii, Wanawake na Watoto ya mwaka 2012/2013 , Waziri Duni alisema waganga wamevamia maeneo ya misikiti na kuuza dawa za kienyeji zinazodaiwa kuongeza nguvu za kiume.




Alisema inashangaza kuna dawa zinazouzwa na za wanaume pekee lakini akasema ni jukumu la wananchi wenyewe kuwa makini kwa vile siyo kila daktari wa tiba asilia anaweza kutibu kila aina ya maradhi.




Hata hivyo,Waziri Duni  alisema kwa upande mwingine, vyombo vya habari vimekuwa vikichangia kuwaingiza wananchi katika matumizi ya dawa ambazo hazijathibitishwa ubora wake kutokana na kutangaza bila kupata ukweli wa dawa hizo.




Alisema baadhi ya dawa zinazouzwa huchangia matatizo ya wagonjwa kutokana na kuzitumia bila  maelekezo ya kitaalam, hivyo wanapozidiwa na kwenda hospitali, ugonjwa huwa mkubwa na wengine kupoteza maisha.




Hata hivyo, Duni alisema ataendelea kusimamia ukweli kwa vile umri wake unafikia ukingoni.




Alisema serikali imeshatunga Sheria ya Afya ya Jamii na Mazingira namba 11 ya mwaka 2012 ambayo itasaidia kuondoa matatizo ya matumizi mabaya ya tiba asilia.




Chanzo: NIPASHE 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad