Azam FC yalazimishwa sare ya bila kufungana na Klabu ya AS FAR Rabat ya Morocco ,katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu ya Kombe la Shirikisho Afrika. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, April 20, 2013

Azam FC yalazimishwa sare ya bila kufungana na Klabu ya AS FAR Rabat ya Morocco ,katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu ya Kombe la Shirikisho Afrika.



Klabu ya Azam FC imelazimishwa sare ya bila kufungana jioni hii(April 20,2013) na  Klabu ya AS FAR Rabat ya Morocco katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu ya Kombe la Shirikisho Afrika  katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



Matokeo hayo yanaifanya Azam FC iwe na mtihani mgumu katika mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo Morocco, wakitakiwa lazima kushinda au kutoa sare ya mabao ili kufuzu.



Pamoja na sare hiyo, Azam FC   watakumbuka sana mabao matatu ya wazi waliyokosa kupitia kwa washambuliaji wao wa pembeni, Kipre Herman Tchetche mawili na Khamis Mcha ‘Vialli’ moja, Kipre aligongesha mwamba mashuti mawili katika dakika za 51 pembeni kushoto katikati  na dakika ya 90+1 mwamba wa juu katikati baada ya jitihada za kuwatoka mabeki wa AS FAR Rabat.



Azam FC 
Khamis Mcha naye alimtoka vizuri beki wa pembeni wa AS FAR Rabat dakika ya 52 lakini akapiga nje shuti lake.



Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Emile Fred wa Shelisheli, aliyesaidiwa na nduguze Steve Maire na Jean Ernesta pembeni, kipindi cha kwanza Azam walionekana kucheza kwa tahadhari zaidi na kufanya mashambulizi machache.




Lakini kipindi cha pili, walifunguka na kuanza kushambulia moja kwa moja jambo ambalo liliweka kwenye misukosuko lango la AS FAR Rabat kwa muda mrefu hadi wachezaji wa timu hiyo kuanza kufanya hila za kupoteza muda ili kupunguza kasi ya wenyeji.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad