Benki ya Dunia kusambaza umeme wa mionzi ya jua (SOLA) Biharamulo Vijijini. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, April 23, 2013

Benki ya Dunia kusambaza umeme wa mionzi ya jua (SOLA) Biharamulo Vijijini.




Solar Panels

Matumizi ya nguvu za jua.
Benki ya Dunia kwa kushirikiana na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) zinatarajia kusambaza umeme wa mionzi ya jua (SOLA) katika zahanati sita na shule sita za sekondari katika vijijini vya Wilaya ya Biharamulo, mkoani Kagera.




Mkurugenzi wa Kampuni ya Kufunga Umeme Vijijini (RESCO),Bw. Mzumbe Mussa amesema hayo jana(April 22,2013) alipokuwa akizungumzia shughuli zinazotarajiwa kutekelezwa na kampuni yake kwenye zahanati na sekondari katika vijiji hivyo.




Alisema hatua hiyo inalenga katika kuwaboreshea mazingira ya kuishi kwa watumishi wa zahanati hizo.




Bw.Mussa alisema lengo la msaada huo ni kuisaidia serikali kuboresha huduma kwa wananchi wa vijijini wanaokabiliwa na changamoto za ukosefu wa nishati ya umeme.




Aidha  alieleza kwamba Benki ya Dunia imekuwa ikishirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii nchini, kutatua baadhi ya changamoto zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.




Zahanati zitakazonufaika na msaada huo ni Kalenge, Nyakanazi, Ngalalambe, Katahoka, Kasozibakaya na Mbindi.




Kwa upande wa wa shule ni za Runazi na Nyantakara.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad