Bayern Munich face Barcelona, Real Madrid against Borussia Dortmund - The prospect of an all-German or an all-Spanish European Champions League final next month -Wembley - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, April 12, 2013

Bayern Munich face Barcelona, Real Madrid against Borussia Dortmund - The prospect of an all-German or an all-Spanish European Champions League final next month -Wembley



Kuna nafasi tunaweza tukashuhudia El Classico kwenye fainali ya ligi ya mabingwa wa ulaya kwenye dimba la Wembley baada ya Real Madrid na Barcelona kutengenishwa kwenye droo ya nusu fainali iliyofanyika muda mchache uliopita jijini Geneva Uswis. 




Kikosi cha Jose Mourinho Real Madrid kimepangwa kucheza dhidi ya Borussia Dortmund wakati Barcelona wamepangwa kucheza na Bayern Munich, hivyo kumaanisha kwamba ikiwa wapinzani wa ligi mbili tofauti - Spain na Ujerumani wanaweza kukutana kwenye fainali ya Wembley May 25.




Dortmund ndio timu pekee ambayo haijapoteza mechi hata moja kwenye michuano hii, na watacheza na Real kwa mara pili ndani ya msimu huu wa UCL. Dortmund waliweza kushinda na kuongoza kundi gumu lilokuwa likihusisha timu za Real, Manchester City na Ajax.




Mabingwa wa sasa wanaosubiri kuvikwa taji tu la Bundesliga  Bayern Munich wapo kwenye form ya kutisha msimu huu, wakitoka kuikanyaga Juventus nyumbani na ugenini.




Mechi za kwanza za nusu fainali ya ligi ya mabingwa wa ulaya zitachezwa April 23 na April 24, na marudiano zitafanyika wiki inayofuatia tarehe April 30 na May 1.




Wakati kwa upande wa UEROPA LEAGUE - Chelsea wamepangwa na FC Basel wakati  Fenerbahce watakipiga na Benfica.




Mechi hizo za Nusu Fainali zitachezwa kwa mtindo wa Nyumbani na Ugenini na Mechi za kwanza zitachezwa Alhamisi Aprili 25 na Marudiano Alhamisi Mei 2.




Fainali itakayochezwa Jumatano Mei 15 ndani ya Amsterdam ArenA kuanzia Saa 3 Dakika 45 Usiku, kwa saa za Africa ya Mashariki.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad