Kundi la Majambazi lateka magari matano na kupora abiria na kisha kuwacharaza viboko katika Kijiji cha Kikoma Kata ya Rusahunga, Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, January 25, 2013

Kundi la Majambazi lateka magari matano na kupora abiria na kisha kuwacharaza viboko katika Kijiji cha Kikoma Kata ya Rusahunga, Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera.


 Kamanda wa Polisi

Mkoa wa Kagera,

Philip Kalangi

Kundi la Majambazi limeteka mabasi matano  mojawapo likiwa la wanajeshi wa Rwanda na kupora abiria na kisha kuwacharaza viboko.


Akithibitisha  tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi  amesema kuwa tukio hilo lilitokea juzi alfajiri  katika Kijiji cha Kikoma kilichoko Kata ya Rusahunga, Wilaya ya Biharamulo.


Mashuhuda wa tukio hilo  wameeleza kuwa majambazi hao wakiwa na silaha za kivita, waliweka kizuizi na kuyasimamisha magari hayo moja baada ya jingine kasha  kuwashusha abiria na kuwapora kila kitu walichokuwa nacho.


Baada ya kuwapora abiria, waliamua kuwacharaza viboko mmoja baada ya mwingine, kisha kutokomea kusikojulikana,” alisema shuhuda mmoja wa eneo hilo ambaye hakutaka jina lake liandikwe na kuongeza.


Magari yaliyotekwa ni Toyota Hiace, gari moja ni la wanajeshi waliokuwa wakitokea Rwanda kwenda Dar es Salaam.”


Diwani wa Kata ya Rusahunga,Bw. Amon Mizengo alisema tukio hilo lilihusisha majambazi wanane waliokuwa na bunduki sita za kivita.


Diwani huyo amesema magari yaliyotekwa yalikuwa yakitokea Ngara na Benaco na kuwa baada ya abiria kuporwa kila kitu, waliamuriwa kuendelea na safari zao.


Kamanda Kalangi amesema Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.


Eneo hilo limekuwa likiripotiwa matukio kadhaa ya ujambazi na mwaka 2007 wabunge wanaotokea maeneo hayo waliomba kuwekwa kwa minara ya mitandao ya simu ili kuwa na mawasiliano.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad