Mabingwa watetezi Real Madrid wamewatandika Atletico Madrid Bao 2-0 kwenye mechi ya Dabi ya Jiji la Madrid huku Bayern Munich na Borussia Dortmund ngoma ngumu kueleweka. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, December 02, 2012

Mabingwa watetezi Real Madrid wamewatandika Atletico Madrid Bao 2-0 kwenye mechi ya Dabi ya Jiji la Madrid huku Bayern Munich na Borussia Dortmund ngoma ngumu kueleweka.

Cristiano Ronaldo
Mabingwa watetezi wa La Liga Real Madrid wamewatandika Atletico Madrid Bao 2-0  kwenye mechi ya Dabi ya Jiji la Madrid  Jumamosi Usiku, na kuwavuta  Atletico Madrid walio nafasi ya pili lakini vinara FC Barcelona wamezidi kujichimbia kileleni  baada ya kuitandika Athletic Bilbao Bao 5-1 kwa bao za  Lionel Messi, Cesc Fabregas, Adriano, Mardaras, kwa kujifunga mwenyewe na bao pekee la Bilbao kufungwa na Gomez.





Aidha Mabao ya Real Madrid yalifungwa na Cristiano Ronaldo kwa frikiki na Mesut Ozil.




LA LIGA.


Matokeo ya Jumamosi Desemba 1


Getafe 1 Malaga 0

Valencia 2 Real Sociedad 5

Barcelona 5 Athletic Bilbao 1

Real Madrid 2 Atletico Madrid 0




MSIMAMO


1 Barcelona Mechi 14 Pointi 40

2 Atletico Madrid Mechi 14 Pointi 34

3 Real Madrid Mechi 14 Pointi 29

4 Malaga Mechi 14 Pointi 22

5 Real Betis Mechi 14 Pointi 22

6 Getafe Mechi 14 Pointi 22




WAFUNGAJI BORA LA LIGA


-Lionel Messi [Barcelona] Magoli 20

-Cristiano Ronaldo [Real Madrid] 12

-Radamel Falcao 11



Bayern Munich

Huko katika BUNDESLIGA Ligi ya Ujerumani, Mabingwa watetezi Borussia Dortmund, wakicheza ugenini Uwanja wa Allianz Arena, walitoka sare na na vinara wa Bundesliga Bayern Munich kwa kufungana Bao 1-1 na kuendelea kushikilia nafasi ya 3 wakiwa Pointi 11 nyuma ya Bayern Munich.


Katika Mechi hiyo, Bayern Munich walitangulia kufunga kwa Bao la Toni Kroos katika Dakika ya 67 lakini Borussia Dortmund wakasawazisha katika Dakika 74 kwa Bao la Mario Goetze.

 

 
MSIMAMO


1 Bayern Munich Pointi 38

2 Bayer Leverkusen 30

3 Borussia Dortmund 27

4 Schalke 25

5 Eintracht Frankfurt 24

 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad