Kocha Arsene Wenger hafikirii kuibwaga Arsenal baada ya vipigo kwa Arsenal na huko Chelsea Benitez akihofia kutimuliwa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, December 02, 2012

Kocha Arsene Wenger hafikirii kuibwaga Arsenal baada ya vipigo kwa Arsenal na huko Chelsea Benitez akihofia kutimuliwa.

Arsene Wenger
Baada ya Mechi za jana za Ligi Kuu soka Uingereza  ambazo zilishuhudia vipigo kwa Arsenal na Chelsea na sare kwa Mabingwa watetezi Manchester City, Mameneja wa Timu hizo wameibuka na kuzungumzia kilichowasibu.




Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger  ametaka Watu wote Arsenal washikamane na kuonyesha wako pamoja.



Arsenal, baada ya kuchapwa 2-0 Jumamosi na Swansea City tena wakiwa kwao Emirates, Mashabikiwa wa Timu hiyo waliizomea Timu yao.



Kipigo hicho kimewafanya Arsenal washuke hadi nafasi ya 10 wakiwa Pointi 15 nyuma ya vinara Manchester United.



Akihojiwa kama anatafakari kung’oka Arsenal, Wenger alisema hafikirii hivyo na tathmini yeyote itafanywa mwishoni mwa Msimu.



Reading 3 Man United 4
Matokeo ya hapo Jana Des 1,2012


West Ham 1 Chelsea 3

Arsenal 0 Swansea 2

Fulham 0 Tottenham 3

Liverpool 1 Southampton 0

Man City 1 Everton 1

QPR 1 Aston Villa 1

West Brom 0 Stoke 1

Reading 3 Man United 4



West Ham.
Nae Meneja wa muda wa Chelsea, Rafael Benitez, amekiri kuwa huenda akafukuzwa baada ya kuiongoza Timu katika Mechi 3 bila ushindi ambazo alitoka sare mbili na Jumamosi kutandikwa 3-1 na West Ham.



Amekiri: “Sina uhakika Asilimia 100 kuhusu hatima yangu. Hatukushinda na hilo ni jambo kubwa!”



Mario Balotelli
Kwa upande wake Meneja wa Mabingwa Manchester City Roberto Mancini  mara baada ya kutoka 1-1 na Everton, amelaumu ubutu wa Mafowadi wake.




Man City sasa wapo nafasi ya pili Pointi 3 nyuma ya vinara Man United na kocha Mancini amewataka kina Dzeko, Tevez, Sergio Aguero na  Mario Balotelli, wachacharike zaidi.



Mechi inayofuata kwa Man City ni dhidi ya Mahasimu wao Man United Uwanjani Etihad Jumapili Desemba 9.




MSIMAMO


1 Man United Pointi  36

2 Man City Pointi  33

3 Chelsea Pointi  26

4 WBA Pointi   26

5 Tottenham Pointi   26

6 Everton Pointi   23

7 Swansea Pointi   23

8 West Ham Pointi   22

9 Stoke Pointi   22

10 Arsenal Pointi   21



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad