Kilimanjaro Stars yafuzu hatua ya Robo Fainali ya michuano ya CECAFA Tusker Challenge kwa kuichapa Somalia mabao 7-0 katika Uwanja wa Lugogo mjini Kampala, Uganda . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, December 01, 2012

Kilimanjaro Stars yafuzu hatua ya Robo Fainali ya michuano ya CECAFA Tusker Challenge kwa kuichapa Somalia mabao 7-0 katika Uwanja wa Lugogo mjini Kampala, Uganda .

Kilimanjaro Stars
Timu ya Tanzania  Bara, Kilimanjaro Stars imefuzu kuingia hatua ya robo fainali ya mashindano  ya CECAFA  Tusker Challenge 2012 , baada ya kuinyuka Somalia  mabao 7- 0 katika  mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Lugogo mjini Kampala nchini Uganda.





Kwa matokeo hayo yanaifanya Kilimanjaro Stars  inayodhaminiwa na TBL kupitia bia ya  Kilimanjaro Premium Lager  ifikishe pointi 6 baada ya kucheza mechi tatu na wakiwa wameshinda michezo miwili na kufungwa mchezo mmoja katika kundi lao la B.




Iliwachukua sekunde 48 tu Kili Stars kupata bao la kwanza, kupitia kwa mshambuliaji wa Simba SC  Mrisho Khlfan Ngassa  aliyewazidi ujanja mabeki wa Somalia huku bao la pili likifungwa  dakika ya 23  na Ngassa tena, aliyeunganisha kona nzuri ya Issa na Rashid.



Mrisho na mpira wake
 baada ya kufunga
mabao matano.
John Bocco ‘Adebayor’ alifunga bao la tatu katika mchezo wa leo na la tatu kwake katika mashindano haya dakika ya 26 akiunganisha kwa kichwa krosi ya Issa Rashid kutoka wingi ya kushoto.



Bocco tena aliwainua vitini mashabiki wa Tanzania kwa kufunga bao la nne kwa kichwa, akiunganisha krosi ya Ngassa dakika ya 41.



Ngassa alifunga bao la tatu katika mchezo wa leo dakika ya 44 na la tano kwa Stars baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na kipa Hussein Abdallah kufuatia shuti kali la Salum Abubakar ‘Sure Boy Jr.’



Somalia ilipata pigo dakika ya 30, baada ya kipa wake namba moja, Mohamed Abdullah kuumia baada ya kugongana na Bocco na kutoka, nafasi yake ikichukuliwa na Hussein Abdallah. 



Bocco
Kipindi cha pili Stars walirejea na moto wao na tena na kufanikiwa kupata mabao mawili zaidi yaliyotiwa kimiani na Ngassa yote dakika za 73 pasi ya Erasto Nyoni na 74 pasi ya Ramadhani Sinago ‘Messi’.




Kwa kufunga mabao matano Mrisho  Ngassa sasa ameingia kwenye mbio za  kuwania kiatu cha dhahabu akikwa anaongoza kwa bao 5, akifuatiwa na Bocco ambaye ana magoli 4  hivi sasa.



Kocha wa Stars, Mdenmark Kim Pouslen baada ya mchezo huo, alisema aliwapongeza vijana wake kwamba wamejitahidi kucheza vizuri na akasifu pia hali nzuri ya Uwanja wa Lugogo kuwa ilichangia ushindi huo.



Katika mchezo mwingine uliopigwa kwenye Uwanja wa Nankurunkuru, Burundi ilishinda 1- 0 dhidi ya Sudan bao hivyo kuongoza Kundi B baada ya kufikisha pointi tisa.



MSIMAMO:




1 Burundi  Pointi  9

2 Kili Stars  Pointi  6

3 Sudan  Pointi 

4 Somalia  Pointi  0



 ROBO FAINALI:




Jumatatu Desemba 3


Mechi Namba 19. Mshindi Kundi C v  Kenya


Mechi Namba 20. Uganda v Mshindi wa 3 Bora wa Pili


Jumanne Desemba 4


Mechi Namba 21. Burundi  v Mshindi wa 3 Bora wa Kwanza


Mechi Namba 22. Mshindi wa Pili Kundi A v Mshindi wa Pili Kundi C



NUSU FAINALI: Desemba 6



Mshindi Mechi Namba 19 na Mshindi Mechi Namba 20


Mshindi Mechi Namba 21 na Mshindi Mechi Namba 22




FAINALI: Desemba 8


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad