Zanzibar Heroes wamejiweka nafasi nzuri kutinga Robo Fainali kutoka Kundi C baada ya kuichapa Rwanda bao 2-1 katika CECAFA TUSKER CHALENJI CUP 2012. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, November 30, 2012

Zanzibar Heroes wamejiweka nafasi nzuri kutinga Robo Fainali kutoka Kundi C baada ya kuichapa Rwanda bao 2-1 katika CECAFA TUSKER CHALENJI CUP 2012.

Rwanda 1 Zanzibar 2
Michuano ya kusaka Nchi Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati  CECAFA TUSKER CHALENJI CUP 2012 inayoendelea huko nchini Uganda, Zanzibar Heroes wamejiweka nafasi nzuri kutinga Robo Fainali kutoka Kundi C baada ya kuichapa Rwanda Mabao 2-1 na kutwaa uongozi wa Kundi hilo.




Magoli  mawili ya Zanzibar yalifungwa na Kiungo wa Azam FC, Khamis Mcha ‘Vialli’ dakika ya 6 na 61 huku  la Rwanda likifungwa na Dadi Birori dakika ya 79.


Katika Mechi nyingine ya Kundi C, Malawi iliifunga Eritrea Bao 3-2 kwa Bao za Chiukepo Msowoya, Miciam Mhone na Patrick Masanjala na yale ya Eritrea kufungwa na Amir Hamad Omary na Yosief Ghide kwa penalti.


Michuano hii itaendelea Ijumaa Novemba 30 kwa Mechi za mwisho za Kundi A kwa Mechi za Kenya v Ethiopia na Uganda v South Sudan.



Wachezaji wa Zanzibar Heroes wakishangilia goli wakati wa mchezo dhidi ya timu ya Rwanda uliochezwa katika Uwanja wa Nelson Mandela uliopo Nambole nchini Uganda katika mashindano ya Cecafa Challenge.

RATIBA/MATOKEO/ MSIMAMO WA KILA KUNDI:



KUNDI A:


Novemba 24:  Ethiopia 1 South Sudan 0, Uganda 1 Kenya 0

Novemba 27: South Sudan 0 Kenya 2, Uganda 1 Ethiopia 0

Novemba 30: Kenya v Ethiopia,  South Sudan v Uganda


MSIMAMO:

[Kila Timu Mechi 2]

1 Uganda Pointi 6

2 Kenya 3 [Tofauti ya Magoli: 1]

3 Ethiopia 3 [Tofauti ya Magoli: 0]

4 South Sudan 0


KUNDI B:


Novemba 25: Burundi 5 Somalia 1, Tanzania 2 Sudan 0

Novemba 28: Somalia 0 Sudan 1, Tanzania 0 Burundi 1

Desemba 1: Sudan v Burundi, Somalia v Tanzania


MSIMAMO:


[Kila Timu Mechi 2]

1 Burundi Pointi 6

2 Kili Stars 3 [Tofauti ya Magoli: 1]

3 Sudan 3 [Tofauti ya Magoli: -1]

4 Somalia 0


KUNDI C:


Novemba 26: Zanzibar 0 Eritrea 0, Rwanda 2 Malawi 0

Novemba 29: Malawi 3 Eritrea 2, Rwanda 1 Zanzibar 2

Desemba 1: Malawi v Zanzibar, Eritrea v Rwanda


MSIMAMO:


[Kila Timu Mechi 2]

1 Zanzibar Pointi 4

2 Rwanda 3 [Tofauti ya Magoli: 1]

3 Malawi 3 [Tofauti ya Magoli: -1]

4 Eritrea 1


Aidha washindi wawili wa juu wa kila Kundi pamoja na Timu mbili zitakazoshika nafasi za 3 Bora zitaingia Robo Fainali.


ROBO FAINALI: Desemba 3 & 4,2012.


NUSU FAINALI: Desemba 6,2012.


FAINALI: Desemba 8,2012.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad