Waziri Mkuu apitisha chekeche kwa wakurugenzi wa halmashauri nchini. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, September 08, 2012

Waziri Mkuu apitisha chekeche kwa wakurugenzi wa halmashauri nchini.



Mizengo Pinda
Waziri  Mkuu Mizengo Pinda amewavua madaraka wakurugenzi sita wa Halmashauri za Wilaya nchini kwa kushindwa kusimamia rasilimali watu, fedha na kutowajibika.

Kutokana na hatua hiyo, Waziri Mkuu Pinda amewateua watu sita kukaimu nafasi hizo na wakurugenzi wapya 14 huku akiwahamisha wakurugenzi 27 kutoka katika vituo vyao vya kazi kwa sababu mbalimbali.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Bi.Hawa Ghasia  amesema wakurugenzi hao walivuliwa madaraka kwa kushindwa kusimamia rasilimali watu na fedha, kusababisha halmashauri kupata hati chafu na uzembe.

Aliwataja wakurugenzi hao waliovuliwa madaraka kuwa ni Willy Njau (Mwanga), Mpangalukela Tatala (Geita), Theonest Nyamhanga (Kishapu), Eden Munisi (Morogoro), Mhando Senyagwa (Kyela) na Nicholaus Kileka (Ngorongoro).

Pia amesema Serikali haitasita kuchukua hatua pale inapobidi ili kuboresha utendaji na kwamba wengine tayari wana kesi na si busara kuwe na mtu anayekaimu zaidi ya miaka mitatu.

Pia amesema hatua za kinidhamu bado zinaendelea na kwamba baadhi ya wakurugenzi hao tayari wamewafikisha kwenye Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa ajili ya hatua zaidi.

Bi.Hawa Ghasia
Waziri huyo aliwataja wakurugenzi wapya walioteuliwa kujaza nafasi hizo kuwa ni Abdalah Kidwanka (Geita), Rutius Bilakwata (Kishapu), Naomi Nko (Magu ), Abdalah Mfaume (Kyela), Twalib Mbasha (Monduli), Henry Ruyagu (Urambo), Adam Mgoyi (Mbarali) na  Estomih Chang’a (Mpanda).

Wamo pia Leti Shuma (Mwanga), Mohamed Maje (Namtumbo) Fulgency Mponji (Moshi), Robert Nehata (Tunduru), Isabela Chilumba (Kahama), Fikiri Malembeka (Sengerema), Paul Malala (Njombe) na Nasib Mbaga (Biharamulo).

Wakurugenzi wanaohamishwa ili kujaza vituo wazi ni Bibie Mnyamagola (Kongwa), Daudi Mayeji (Kilindi), Protace Magayane (Nkasi), Saada Mwaruka (Mkuranga), Sipora Liana(Tabora Manispaa), Hadija Makuwani (Wilaya ya Tabora), Doroth Rwiza (Kasulu).

Wengine ni Kelvin Makonda (Manispaa ya Lindi), Pudenciana Kisaka (Iringa), Tina Sekambo (Makambako), Beatrice Dominick (Masasi), Gladyness Ndyamvuye (Bukoba), Nathan Mshana (Ngorongoro), Cornel Ngudungi (Ngara), Mohamed Mkupete (Mtwara Manispaa), Dk Koroine Ole Kuney (Misungwi).

Wamo pia Ephraem Ole Nguyaine (Rorya), Goody Pamba (Igunga), Fidelis Lumato (Ludewa), Athuman  (Tarime) na Ahmad Sawa (Musoma Manispaa).

Waliohamishwa kwenda kwenye halmashauri mpya ni Magreth Nakainga (Geita), Eliza Bwana (Bariadi), Zuberi Mbyana, Ilemela Manispaa (Biharamulo), Mohamed Nanyanje (Masasi), Erica Musika (Kahama), Imelda Ishuza (Busokelo).



IMETOLEWA NA


MHE. HAWA A. GHASIA (MB)
WAZIRI WA NCHI - OFISI WAZIRI MKUU
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad