Hongereni Wananchi wa Nyakanazi Biharamulo kwa Ushirikiano Katika Kutekeleza Miradi ya Maendeleo - Waziri Jaffo. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Wednesday, August 15, 2018

demo-image

Hongereni Wananchi wa Nyakanazi Biharamulo kwa Ushirikiano Katika Kutekeleza Miradi ya Maendeleo - Waziri Jaffo.

.com/simgad/
38936139_1920804881274563_5364269777378344960_n
Na: Sylvester Raphael.

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Seleman Jaffo awapongeza wananchi wa Kata ya Nyakanazi Wilayani Biharamulo Mkoani Kagera kwa ushirikiano wao wa kuchangia na kushiriki katika kutekeleza miradi ya maendeleo hasa ujenzi wa Kituo cha Afya Nyakanazi ambacho kimekamilika ujenzi wake baada ya Seriakli kutoa Shilingi milioni 500 ili kiweze kuboreshwa na kutoa huduma muhimu za afya kwa wananchi.

Waziri Jaffo aliyasema hayo Agosti 9, 2018 alipofanya ziara ya siku moja na kutembelea na kukagua ujenzi wa kituo hicho ambapo alisema kuwa amaeridhishwa na ujenzi ulivyofanyika kuwa ni kiwango kinachoridhisha na thamani ya fedha iliyotolewa inaonekana katika majengo yaliyojengwa na mengine kukarabaitiwa.

Nawapongeza wananchi wa Kata ya Nyakanazi kwa kujitoa kushirikiana na Serikali kuhakikisha kituo hiki cha Nyakanazi kinajengwa na kukamilika, nyinyi wananchi mmekuwa mstari wa mbele kutekeleza wajibu wenu pale mlipotakiwa kufanya hivyo na ndiyo maana kituo chenu kimekalika.” Alifafanua Waziri Jaffo.
38797485_1920805324607852_8235465082725728256_n
Waziri Jaffo alizidi kusisitiza kuwa nia ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wake wananpata huduma bora hasa akinamama wajawazito katika suala la upasuaji wakati wa kujifungua sasa tatizo hilo limefika mwisho baada ya kituo hicho kukamilika.
38829188_1920805244607860_1244552819390808064_n

38856420_1920805351274516_7743926171850506240_n
 Aidha, Waziri Jaffo aliongeza kuwa Serikali baada ya kuridhishwa na ujenzi ulivyotekelezwa katika kituo hicho imetoa tena shilingi milioni 400 nyingine za kujenga kituo kingine katika Halmashauri ya Wilaya Hiyo ya Biharamulo.

Pamoja na kuupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo Waziri Jaffo alitoa tahadhari kwa Halmashauri hiyo kusimamia mapato ambapo alisema Biharamulo haifanyi vizuri katika kukusanya mapato.

Pia aliagiza kuitishwa kwa Balaza Maalum la Madiwani ili kujadili ripoti ya Tume ya uchunguzi ilioundwa kuchunguza mapato yanavuja wapi na kama ikigundulika kuna watumishi waliohusika wachukuliwe hatua mara moja naye apewe taarifa.
 38897676_1920804941274557_2439768022307569664_n

39000238_1920805517941166_8153505780889288704_n
Kituo cha Nyakanazi kimekamilika ujenzi wake kwa jumla ya shilingi milioni 700 ikiwa shilingi milioni 500 zilitolewa na Serikali kujenga majengo ya Wodi ya akinamama na watoto, Wodi ya watoto, chumba cha kuhifadhi maiti, Nyumbambili (Two in one) za watumishi na kukarabati chumba cha upasuaji. 

Pia shilingi milioni 200 zilitumika kununua vifaa katika kituo hicho.

Waziri Jaffo alimaliza kwa kusema kuwa Serikali itajenga vituo vyote vya afya Wilayani Biharamulo ili wananchi wote wapate huduma safi, pia alisema wakati Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani mwaka 2015 kulikuwa na Vituo vya Afya 115 tu lakini hadi sasa vimejengwa vituo 210 na tayari vituo 97 vimepewa fedha kujengwa, hayo ni mafanikio na mapinduzi makubwa katika Sekta ya Afya.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *