![]() |
Hivi karibuni
Mkuu wa mkoa wa Kagera alionya kuhusu zao la Kahawa akisema, “Msimamo wangu mimi Mkuu wa Mkoa wa
Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu Kuhusu zao la Kahawa ni kuwa sipo
tayari kuruhusu zao la kahawa liuzwe kwa njia za magendo.
Nitahakikisha
namchukulia hatua kali za Kisheria yeyote yule atakayeweka kikwazo kwa Mkulima
kuuza kahawa yake kupitia Vyama vya Ushirika.
Viongozi
wa Vyama vya Ushirika kuweni makini na kila shilingi ya mkulima Mtambue kuwa
Serikali ipo kazini inafuatilia kila kitu kinachofanyika ndani ya Vyama vyenu.
Hatutasita kuchukua hatua muda na wakati wowote mkicheza na fedha ya Wakulima.
Mtazamo
na furaha yangu nataka kuona Mkulima anatajirika, ana fedha mfukoni kutokana na
zao la Kahawa na lazima Vyama viwe mkombozi wa wakulima na si wanyonyaji wa
Wakulima.” Mkuu wa Mkoa
Mhe. Kijuu
|
Tuesday, July 24, 2018

RC Kagera –‘’Sipo tayari Kuruhusu Zao la Kahawa liuzwe kwa Njia za Magendo.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment