Arsenal yatupwa nje ya michuano ya UEFA Europa League. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, May 04, 2018

Arsenal yatupwa nje ya michuano ya UEFA Europa League.

Arsenal imetupwa nje ya michuano ya UEFA Europa Legua kwa kuchapwa bao 1-0 dhidi ya Atletico de Madrid ya Hispania.

Mshambuliaji Diego Costa akiinua mkono wake juu kushangilia baada ya kuifungia bao pekee Atletico Madrid dakika ya 45 na ushei katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Arsenal usiku May 3, 2018 kwenye Uwanja wa Wanda Metropolitano mjini Madrid, Hispania.

Ulikuwa ni mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali ya Europa League na Atletico Madrid inaingia fainali kwa ushindi wa jumla wa 2-1 baada ya sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza London wiki iliyopita na itamenyana na Olympique Marseille iliyoitoa Red Bull Salzburg ya Austria kwa jumla ya mabao 3-2, ikishinda 2-0 Ufaransa na kufungwa 2-1 ndani ya dakika 120 Wals-Siezenheim.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad