Bilionea
Mohammed Dewji, amepita katika mchakato wa uwekezaji wa klabu ya Simba SC na ofa
yake ya Sh bilioni 20.
Dewji
amejitokeza na kuwa muwekezaji pekee ambaye aliweka dau la Sh bilioni 20 kupata
hisa asilimia 51.
Hata hivyo,
baada ya mchakato huo makubaliano yalikuwa ni hisa 49 anazoruhusiwa kuchukua
kwa kitita hicho cha Sh bilioni 20.
Mwenyekiti
wa kamati ya mchakato huo wa mabadiliko, Jaji Mihayo amesema, Mo Dewji amepita
na kitachofuatia ni majadiliano mengine baada ya mkutano wa leo December 3,
2017.
“Mohammed
Dewji ndiye mshindi, maana katika kamati yetu. Hivyo yeye ndiye amekuwa mshindi
wa kuwania kuwekeza katika klabu ya Simba SC. Baada ya mkutano huu kutakuwa na
majadiliano,” alisema.
Mkutano huo
wa wanachama bado unaendelea Posta jijini Dar es Salaam.
|
No comments:
Post a Comment