![]() |
|
Ni mechi ya
tatu Yanga wanatoka sare katika ligi ikiwa ni mechi ya tano tangu kuanza kwa
ligi msimu huu. Wanajangwani walitoka sare kwa mara ya kwanza dhidi ya Lipuli
kwenye mechi ya ufunguzi walipolazimisha sare ya kufungana 1-1.
|
![]() |
|
Mechi za leo
sare zimetawala kwa asilimia 90 katika Katika
mechi saba zilizochezwa leo ni mechi moja tu ambayo kumekuwa na ushindi huku
sita zote zikiwa ni sare.
Mechi pekee
iliyokuwa na ushindi ni ile Ndanda FC ikiwa nyumbani imefanikiwa kuiripua
Lipuli kwa mabao 2-1.
Lakini
nyingine sita, sare zimechukua nafasi ukianza na sare ya 0-0 kati ya Yanga SC
dhidi ya Mtibwa Sugar.
DODOMA:
Azam FC
ikiwa ugenini dhidi ya Singida United, imelazimisha sare ya 1-1 baada ya
kusawazisha.
MWADUI:
Nayo Mwadui
FC ikiwa nyumbani iemshindwa kuulinda ushindi wake kwa kuiachia Mbeya City
isawazishe na matokeo kuwa 2-2.
MWANZA:
Pamoja na
kuonyesha wako vizuri, Mbao FC nao wameokoka wakiwa nyumbani CCM Kirumba baada
ya kusawazisha katika mechi dhidi ya Prisons iliyotangulia kufunga.
Dakika 90
zimeisha 1-1.
SONGEA:
Majimaji
wakiwa kwenye Uwanja wa nyumbani wa Majimaji mjini Songea wametoka uwanjani kwa
sare ya 0-0 dhidi ya Kagera Sugar.
PWANI:
Ruvu
Shooting walio nyumbani, nao wameshindwa kupata ushindi baada ya Njombe Mji
kuamka na kusawazisha na matokeo ya dakika 90 yakawa 1-1.
|








No comments:
Post a Comment