![]() |
| Kushoto ni Mmiliki wa Mtandao huu Mohamed Makonda aka Mwana wa Makonda katika pozi la picha na Mkurugenzi wa Jambo Bukoba mkoani Kagera Steven Gonzaga mara baada ya Mafunzo kufungwa katika Shule ya Msingi Njia Panda-Benaco. |

![]() |
|
Mafunzo hayo
ambayo yamefanyika katika shule ya msingi Njia Panda ,kata ya Kasulo wilayani
Ngara yamefungwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilkaya ya Ngara , Aidan Bahama
na kuwaagiza Wakuu wote Shule za Msingi
pamoja na Walimu wao wa Michezo kuandaa mpango kazi utakaonesha namna michezo
mbalimbali itakavyofundishwa na kuchezwa katika shule zao.
|

![]() |
|
Hapa
mchezo wa kumtambua kwa macho Mtu mwenye UKIMWI Ukichezwa na Washiriki
ambapo mtu husimama mbele yao na kuambiwa amguse Mtu aliye na kijiti
nyuma kama picha inavyoonesha .
|


![]() |
| Picha Juu na chini mchezo wa kuokota kijiti,kisha unakimbia na kwenda kuandika neneo UKIMWI UPO ,unakuza Ubunifu,Kujiamini,Ushirikiano na Wepesi katika kukimbia. |




![]() |
| Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera Aidan Bahama akikagua Maandishi ya Neno UKWIMI UPO yaliyoandikwa na Washiriki wa mafunzo ya Jambo Bukoba wakati wa hafla ya kufungwa September 16,2017. |


![]() |
| Pichani juu na chini Washiriki wakicheza mchezo wa kuunda umbo la pembe tatu kwa kutumia Kamba. |


![]() |
| Kutoka kulia ni Steven Ngonzaga Mkurugenzi wa Shirika la Jambo Bukoba wakifurahia wimbo uliokuwa ukiimbwa wa Jambo Bukoba sambamba na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera Aidan Bahama , Pembeni yake ni Afisa Michezo wilaya Said Salumu na Mratibu Elimu Kata ya Kasulo. |
![]() |
| Kulia ni Diwani wa Kata ya Kasulo Dr Philbert Kiiza akiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera Aidan Bahama Katikati na Mratibu Elimu kata hiyo kushoto. |

![]() |
|
Kwa upande
wake Mkurugenzi wa shirika la Jambo Bukoba mkoani Kagera Steven Gonzaga Pichani, ametoa
wito kwa Viongozi wa Kiserikali,Chama na Wadau wengineo kuhakikisha wanahamasisha michezo inayofundishwa
na Shirika hilo,inachezwa wakati wote mashuleni ili kutimiza lengo la Mafunzo
ambayo yamekuwa yakitolewa kwa Walimu wa Michezo wa Shule za Msingi mkoani Kagera.
|
![]() |
| Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera Aidan Bahama akisoma
kitabu cha Muongozo wa Mafunzo ya Jambo Bukoba wakati wa hafla ya
kufungwa kwa Mafunzo Jumamosi September 16,2017 katika Shule ya Njia
Panda ,Kata ya Kasulo wilayani Ngara.
|


![]() |
|
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera Aidan Bahama akigawa Cheti kwa Mwalimu aliyehitimu Mafunzo..
Said Salumu
ni Afisa Michezo wilaya ya Ngara na Philbert Kiiza , Diwani wa kata ya Kasulo wamesema
kuwa baada ya Walimu hao wa Michezo 26
kutoka kata Kasulo,Rusumo na Nyakisasa kupata mafunzo hayo,watahakikisha
wanawafatilia na kutoa ushirikiano wa kutosha ili kufikiwa mafanikio ya michezo
mashuleni.
Nao Walimu
waliozungumza na Mtandao huu wameahidi kuwa mabalozi wazuri mashuleni kwako kwa
kuandaa mpango kazi wa michezo utakaohakikisha Wanafunzi wanacheza michezo
mbalimbali ili Kujenga na kukomaza afya ya mwili na akili;Kujenga ukakamavu,
nidhamu na Kuonyesha uwezo na vipaji vya washiriki na Kukuza na kuendeleza
uhusiano wa kirafiki baina ya Shule mbalimbali.
|



















No comments:
Post a Comment