Huu ndio Ufafanuzi wa Ofisi ya Bunge kuhusu Mbowe kunyang’anywa gari-Kenya. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, September 28, 2017

Huu ndio Ufafanuzi wa Ofisi ya Bunge kuhusu Mbowe kunyang’anywa gari-Kenya.

Ofisi ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania -Dodoma  imetoa taarifa kuhusu Mwenyekiti wa CHADEMA –Mhe.Freeman Mbowe kunyang’anywa na Bunge gari lake alilokua analitumia kwenye shughuli mbalimbali za kumuhudumia Tundu Lissu mjini Nairobi nchini Kenya.

Ofisi ya Bunge imesema ililazimika gari hilo lirudishwe Tanzania na kuegeshwa kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha kwa  sababu Dereva wake hakua amekamilisha taratibu za kiofisi kama inavyotakiwa hivyo sasa hivi yuko Dodoma kuzikamilisha.

Awali CHADEMA ilisema Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, aliamuru gari hilo lipelekwe Nairobi kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Lissu ambaye ni Mwanasheria mkuu wa chama hicho.

Lissu ambaye pia Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), alishambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi Septemba 7 akiwa nyumbani kwake Area D mjini Dodoma na yuko Nairobi kwa matibabu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad