MATOKEO / RATIBA VPL 2015/2016:-Ndanda FC waikazia Azam FC huku Coastal Union ikipigwa 2-0. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, April 06, 2016

MATOKEO / RATIBA VPL 2015/2016:-Ndanda FC waikazia Azam FC huku Coastal Union ikipigwa 2-0.

Ndanda FC
Timu ya Ndanda FC ya mkoani Mtwara imeikazia Azam FC na kuilazimisha sare ya kufungana magoli 2-2 kwenye mchezo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa leo April 06,2016 kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
 
Azam FC walianza kupata bao dakika ya 16 kipindi cha kwanza kupitia kwa Ramadhani Singano ambaye aliunganisha pasi ya Michael Balou kabla ya Didier Kavumbagu kutupia kambani bao la pili muda mfupi kabla ya kwenda mapumziko.

  Mchezaji, Atupele Green alizifungua nyavu za Azam FC kwa kuusukuma mpira kambani kwa mkwaju wa penati baada ya golikipa wa Azam FC, Aishi Manula kumwanusha Paul Ngalema kwenye eneo la hatari wakati akijaribu kuokoa hatari golini kwakwe.
 
Bao la kusawazisha la Ndanda FC lilikuwa ni la kujifunga ambapo beki wa Azam FC Agrey Morris aliugonga mpira uliokuwa unaelekea goli na kuubadilisha mwelekeo kisha kumshinda golikipa Aishi Manula na kuzama wavuni.
 
Matokeo hayo ni habari njema kwa Yanga SC na Simba SC ambazo timu zote hizo tatu zinaongoza mbio za kuwania ubingwa wa ligi msimu huu.
 
Matokeo hayo yanaifanya Azam FC ijiongezee pointi moja na kufikisha 52 baada ya kucheza mechi 23, wakiwa nafasi ya tatu nyuma ya mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 53 za mechi 22, wakati Simba SC inaongoza kwa pointi zake 57 za mechi 24.
 
Baada ya mchezo huo, Azam FC inarejea kambini kujiandaa na mchezo wake wa kwanza hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Esperance ya Tunisia Jumapili mjini Dar es Salaam.
 
Mchezo mwingine wa Ligi Kuu leo, wenyeji Majimaji FC wameifunga 2-0 Coastal Union Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
 
Baada ya Mechi za Leo, VPL itaendelea tena Jumamosi April 09,2016.
 
LIGI KUU VODACOM  TANZANIA BARA 2015/2016 – RATIBA.    

 

Jumamosi Aprili 09,2016.


Ndanda FC v Mwadui FC 


African Sports v Kagera Sugar   


Mtibwa Sugar v Tanzania Prisons


Jumapili Aprili 10,2016.


Mgambo JKT v Mbeya City


Jumatatu Aprili 11, 2016.


Toto Africans v Majimaji  


Jumatano Aprili 13, 2016.


Mtibwa Sugar v Azam FC


Yanga v Mwadui FC


Jumamosi Aprili 16, 2016.


Coastal Union v JKT Ruvu


Yanga v Mtibwa Sugar    


Jumapili Aprili 17, 2016.


Simba SC v Toto Africans


Jumatano Aprili 27, 2016.


Azam FC v Majimaji


Yanga v Mgambo JKT     


Jumamosi Aprili 30, 2016.


Toto Africans v Yanga     


Simba SC v Azam FC      


Ndanda FC v Kagera Sugar


African Sports v Coastal Union  


Mwadui FC v Stand United


Mtibwa Sugar v Mbeya City       


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad