MATOKEO / RATIBA EPL 2015/2016:-West Ham 3-3 Arsenal. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, April 09, 2016

MATOKEO / RATIBA EPL 2015/2016:-West Ham 3-3 Arsenal.

Arsenal Westham (21)

Mabao 3 ndani ya Dakika 9 ya mchezaji wa West Ham Andy Carroll, Leo April 9, 2016 huko Upton Park imekuwa pigo kubwa kwa Arsernal katika mbio zao za Ubingwa wa Ligi Kuu walipotangulia 2-0 na kuambua Sare ya 3-3 na West Ham.


Arsenal walipata Bao lao la kwanza Dakika ya 18 baada ya pasi ya Iwobi kumkuta Mesut Ozil aliemalizia vizuri na la pili kufungwa Dakika ya 35 kupitia Alexis Sanchez kwa pasi iliyotoka kwa Iwobi.

Arsenal Westham (22)
Arsenal Westham (23)
Arsenal Westham (25)
Arsenal Westham (26)Arsenal Westham (27)Arsenal Westham (28)Arsenal Westham (29)Arsenal Westham (30)Arsenal Westham (31)


West Ham walifufuka na kufunga Bao lao la kwanza Dakika ya 44 kwa Kichwa cha Andy Carroll alieunganisha krosi ya Cresswell na kupata Bao la Pili Dakika ya 47 kupitia tena Andy Carroll ambae aliunganisha Mpira wa Kona iliyoooshwa na kumkuta Mark Noble alieurudisha tena Golini na kumkuta Carroll aliepiga Shuti la kwanza ambalo lilizuiwa na kuachia kigongo cha pili na kumparaza Beki na kumhadaa Kipa Ospina.

Dakika ya 52 Carroll alipiga Bao la 3 na kukamilisha Hetitriki yake ya ndani ya Dakika 9 tu.

Arsenal walisawazisha na kuambua Sare ya 3-3 katika Dakika ya 70 kwa Bao la Laurent Koscielny.

Matokeo haya yamezibakisha Arsenal Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 10 nyuma ya Vinara Leicester City na West Ham kuwa Nafasi ya 6.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad