KLABU BINGWA ULAYA:- Mtu 10 Atletico Madrid wafungwa 2-1 Barcelona. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, April 06, 2016

KLABU BINGWA ULAYA:- Mtu 10 Atletico Madrid wafungwa 2-1 Barcelona.

Mabingwa Watetezi wa Klabu Bingwa Ulaya, FC Barcelona wakiwa kwao Nou Camp Jijini Barcelona Nchini Hispania, wamewafunga  Atletico Madrid magoli  2-1 katika Mechi ya kwanza ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa,iliyochezwa  Jana April 05,2016,usiku.

Fernando Torres alliipa goli la kuongoza  Atletico Dakika ya 26 lakini akapewa Kadi ya Njano Dakika ya 30 na kuizoa nyingine Dakika ya 37 na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Katika mchezo huo,FC Barcelona walisawazisha Dakika ya 63 pale shuti la Neymar kuelekea Golini lilipomaliziwa kibahati na Luis Suarez.

Dakika ya 74 Luis Suarez tena akaona nyavu kwa Kichwa kufuatia Krosi ya Dani Alves na kuwapa Barca ushindi wa 2-1.

Matokeo hayo, yanamaanisha Barcelona bado haipo salama, kwani inaweza kutolewa iwapo itafungwa 1-0 katika mchezo wa marudiano mjini Madrid.

Robo Fainali za pili zitachezwa Leo,April 06,2016 kwa VfL Wolfsburg na Real Madrid Uwanja wa Volkswagen Arena na Paris Saint-Germain dhidi ya Manchester City Uwanja wa Parc des Princes.

Jumatano Aprili 06,2016.

Paris St-Germain v Manchester City

Wolfsburg v Real Madrid

Marudiano

Jumanne Aprili 12,2016.

Manchester City v Paris St-Germain

Real Madrid v Wolfsburg

Jumatano Aprili 13,2016.

Benfica v Bayern Munich

Atletico Madrid v Barcelona

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad