RATIBA / MATOKEO VPL 2015/2016:-SimbaSC yarudi kileleni mwa Ligi wakiitoa Yanga SC …ikishinda 3 – 0 dhidi ya Ndanda FC. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, March 10, 2016

RATIBA / MATOKEO VPL 2015/2016:-SimbaSC yarudi kileleni mwa Ligi wakiitoa Yanga SC …ikishinda 3 – 0 dhidi ya Ndanda FC.

Hamisi Kiiza akishangilia goli lake la kwanza dhidi ya Stand United kwenye uwanja wa Kambarage Shinyanga

    Kiiza (Pichani ) amefikisha mabao 18 baada ya kufunga bao mbili kwenye mchezo kati ya Simba dhidi ya Ndanda FC. Kiiza anamzidi Amis Tambwe wa Yanga mwenye mabao 17 aliyofikisha baada ya kufunga magoli mawili wakati Yanga SC iliposhinda kwa magoli 5-0 dhidi African Sports. 


‘Wekundu wa Msimbazi’ Simba SC wameendelea kufanya Vyema  kwenye Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara Msimu huu 2015/2016,kufuatia ushindi mnono wa magoli 3 - 0 dhidi ya Ndanda FC ya Mtwara kwenye mchezo wao wa marudiano uliochezwa kwenye uwanja wa taifa,Jijini Dar es Salaam leo March 10, 2016,Jioni.



Simba SC  ilianza kupata bao la kwanza lililofungwa na Mwinyi Kazimoto dakika ya 32 akiunganisha vizuri krosi ya Ibrahim Ajib huku Dakika ya 52 Kiiza angafunga bao la pili ambalo lilikuwa ni bao lake la 17 kwenye Ligi, Kiiza aliunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Ibrahim Ajib.



Kiiza aliifungia Simba SC bao la tatu na kuchukua usukani wa wafungaji bora wa VPL baada ya kuunganisha pasi ya Danny Lyanga aliyeuwahi mpira uliotemwa na golikipa wa Ndanda kufuatia shuti kali la mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Justice Majabvi.



SimbaSC  imefikisha jumla ya pointi  51 baada ya kucheza michezo 22 na kurudi kileleni mwa ligi kwa mara nyingine wakiitoa Yanga SC yenye pointi 50 ikiwa imecheza michezo 21.
Mwadui


Mchezo mwingine wa Ligi Kuu leo,March 10,2016  Mbeya City Imeifunga 2-0 Stand United Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, mabao ya Raphael Daudi na Haruna Shamte.

Matokeo yote ya mechi za VPL zilizochezwa March 09, 2016, yapo kama ifuatavyo.



Mwadui FC 0 - 0 Majimaji FC



Tanzania Prisons 1 - 1 Kagera Sugar



Coastal Union 1 - 0 Mgambo JKT



JKT Ruvu 2 - 0 Toto Africans

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad