ZIARA MIKOA YA MWANZA, GEITA NA KAGERA:- Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amsimamisha kazi Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na nyumba wilaya ya Chato Mkoani Geita. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, February 26, 2016

ZIARA MIKOA YA MWANZA, GEITA NA KAGERA:- Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amsimamisha kazi Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na nyumba wilaya ya Chato Mkoani Geita.

mab01
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline Sylvester Lubala Mabula akisalimiana na Watumishi wa Hamashauri ya Mji wa Buchosa alipowasili kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi.
MAB1
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline Sylvester Lubala Mabula akipewa maelezo na mtaalam wa mifumo ya uwekaji kumbukumbu za umiliki wa ardhi alipotembelea idara ya ardhi Wilayani Misungwi. Aliyoko katikati ni Mkurugenzi wa Halmshauri hiyo Bw. Mshana.

MAB2
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline Sylvester Lubala Mabula na Mbunge wa Chato Mhe.Dkt Medard Kalemani wakikagua eneo la Kijiji cha Rusungwa lenye mgogoro mkubwa wa ardhi unaofanya wananchi wa kijiji hicho kukosa ardhi ya kulima na uwekaji huduma za jamii kama shule baada ya eneo la ekari 500 la kupewa mwekezaji.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline Sylvester Lubala Mabula,amemsimamisha kazi Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na nyumba wa wilaya ya Chato Mkoani Geita Bw Emmanuel Mogasa ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili

Uamuzi huo ameutoa  Juzi ,February 24,2016 katika ziara ya Kikazi ya Siku 2 wilayani Chato Mkoani Geita ambapo alimtaka Msajili wa Mabaraza ya Ardhi wa Kanda ,Bi Doroth Philip kupeleka haraka Mwenyekiti mwingine wa Baraza la Ardhi wilayani humo ili wananchi waendelee kupata huduma

Amesema Mwenyekiti huyo amekuwa akilalamikiwa na Wananchi kwa muda mrefu kutokana na kukithiri kwa vitendo vya rushwa, kufanya kazi kwa mazoea, kuchelewesha maamuzi ya kesi na kupindisha haki katika baadhi ya migogoro

Baadhi ya wakazi wa Chato wameonekana kupokea uamuzi huo kwa hisia tofauti ambapo Bw Mateso Misana amepongeza uamuzi huo huku Bw Cosmas Edward akisema kuwa Haki haijatendeka kwa madai kuwa karibu Mabaraza yote nchini yamekuwa yakilalamikiwa kwa kutotenda haki

Katika Ziara hiyo Pia ,Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline Sylvester Lubala Mabula  ameagiza Halmashauri kushughulikia migogoro ya ardhi, Azitaka kulisaidia Shirika la Nyumba ili lijenge nyumba za gharama nafuu sambamba na Halmashauri zinunue nyumba zinazojengwa na NHC kwa ajili ya watumishi wao.

 Alipongeza NHC kwa kasi ya ujenzi wa nyumba bora katika Halmashauriza Miji na Wilaya.


Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na Mimi Hapa...FACEBOOK .. TWITTER .. INSTAGRAM … Pia Usisite kututumia tukio la Picha/Habari  kwa WhatsApp +255789925630  Or  +255756830214.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad