TANZIA:-Mwanamuziki Mkongwe Kassim Kapili Afariki Dunia. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, February 26, 2016

TANZIA:-Mwanamuziki Mkongwe Kassim Kapili Afariki Dunia.

7a
Mwanamuziki mkongwe wa muziki dansi Kassim Mapili akicharaza nyuzi za Gitaa lake chini ya Kundi zima la Mjomba Band.

MWANAMUZIKI mkongwe wa muziki Dansi Nchini Tanzania, Kassim Mapili amefariki dunia akiwa chumbani kwake, Tabata jijini Dar es Salaam. 

Katibu mkuu wa Chama cha Muziki wa Dansi (CHAMUDATA) Hassan Msumari, amesema kuwa kifo cha Mapili kimegunduliwa usiku wa Jana February 25,2016 baada ya mlango wa chumba chake kuvunjwa.

 Mlango huo ulivunjwa baada ya Kassim Mapili kutoonekana tangu alipokwenda kutazama mpira wa Arsenal na Barcelona Jumanne,February 23,2016, usiku.

Kwa mujibu wa Msumari, mara mlango ulipovunjwa Kassim Mapili alionekana akiwa ameshafariki akiwa amejifunga taulo, ishara inayoonyesha kuwa aidha alikuwa anakwenda kukoga au ametoka kukoga.

Jumatatu jioni Kassim Mapili alishiriki vizuri mazishi ya mwanahabari Fred Mosha makaburi ya Kinondoni ambapo alipewa wasaa wa kuongea machache na kama vile hiyo haitoshi, Mapili aliimba makaburini hapo kuomboleza kifo cha Fred Mosha.
 
 
(CREDIT: SAID MDOE)
 
Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na Mimi Hapa...FACEBOOK .. TWITTER .. INSTAGRAM … Pia Usisite kututumia tukio la Picha/Habari  kwa WhatsApp +255789925630  Or  +255756830214.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad