KLABU BINGWA ULAYA:- Dynamo Kiev yalizwa na Manchester City 3 -1 .. PSV Eindhoven na Atletico Madrid sare. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, February 25, 2016

KLABU BINGWA ULAYA:- Dynamo Kiev yalizwa na Manchester City 3 -1 .. PSV Eindhoven na Atletico Madrid sare.

Jana February 24,2016, Manchester  imejiweka vyema kutinga Robo Fainali baada ya kupata ushindi mnono Ugenini katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UEFA CHAMPIONZ LIGI 2015/2016 walipoichapa Dynamo Kiev Bao 3-1 huko Kiev, Nchini Ukraine.

Man City, ambao walibadili Wachezaji 10 toka kile Kikosi kilichodundwa 5-1 na Chelsea kwenye FA CUP Jumapili iliyopita, walitawala Kipindi cha Kwanza na kupiga Bao 2 kupitia Sergio Aguero na David Silva zilizofungwa Dakika za 15 na 40.

Vitaliy Buyalsky aliipa Bao Dynamo katika Dakika ya 58 na Gemu kuwa 2-1 lakini Yaya Toure akawakata maini katika Dakika ya 90 kwa Shuti murua la kupinda na kufunga Bao la 3 na kuwapa City ushindi mnono wa 3-1 kuelekea Mechi yao ya Marudiano hapo Machi 15 Uwanjani Etihad.

Katika Mechi nyingine ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UCL PSV Eindhoven na Atletico Madrid zilitoka Sare 0-0 huko Mjini Eindhoven Nchini Uholanzi.

PSV walibaki Mtu 10 kuanzia Dakika ya 58 baada ya Pereiro kupewa Kadi Nyekundu kufuatia Kadi za Njano 2.

UEFA CHAMPIONZ LIGI 2015/2016 -RAUNDI YA MTOANO YA TIMU 16

Marudiano

JUMANNE 08 MAR 2016

Real Madrid v AS Roma [2-0]

VfL Wolfsburg v KAA Gent [3-2]

JUMATANO 09 MAR 2016

2000 Zenit St Petersburg v Benfica [0-1]

Chelsea v Paris St Germaine [1-2]

JUMANNE 15 MAR 2016

Atletico Madrid v PSV Eindhoven [0-0]

Man City v Dynamo Kiev [3-1]   

JUMATANO 16 MAR 2016

Barcelona v Arsenal [2-0]

Bayern Munich v Juventus [2-2]

 Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na Mimi Hapa...FACEBOOK .. TWITTER .. INSTAGRAM … Pia Usisite kututumia tukio la Picha/Habari  kwa WhatsApp +255789925630  Or  +255756830214.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad