MGOMBEA JIMBO LA HANDENI:- CCM Yaanza mchakato wa kumtafuta. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, November 03, 2015

MGOMBEA JIMBO LA HANDENI:- CCM Yaanza mchakato wa kumtafuta.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akizungumza na wanahabari (hawapo pichani).

Picha ya juu na chini ni  Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini mkutano huo.


Nape akijiandaa kujibu maswali ya wanahabari yaliyokuwa yameulizwa (hawapo pichani).

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema kipo kwenye mchakato wa kumtafuta mgombea wake wa Ubunge Jimbo la Handeni mkoani Tanga baada ya kutofanyika uchaguzi kufuatia kifo cha mgombea wake kwa tiketi ya chama hicho, Abadallah Kigoda.

Akizungumza na wanahabari November 02,2015, kwenye ofisi za chama hicho zilizopo mtaa wa Lumumba jiijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye amesema kuwa, wajumbe wa kamati ya CCM wapo kwenye mchakato huo na kesho mgombea atapatikana.

Alisema kamati hiyo imeshachuja waliojitokeza kuomba nafasi hiyo ambao walikuwa 11 na sasa wamebaki wawili ambao ni Hamis Hamad na Omar Kigoda hivyo kesho watakaa kikao cha kumpata mgombea mmoja.

NA DENIS MTIMA/GPL

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad