Matokeo ya uchaguzi wa urais Tanzania | |||
---|---|---|---|
Jina | Chama | Kura | Asilimia |
Anna Mghwira | ACT | 98,763 | 0.65 |
Chifu Yemba | ADC | 66,049 | 0.43 |
John Magufuli | CCM | 8,882,935 | 58.46 |
Edward Lowassa | CHADEMA | 6,072,848 | 39.97 |
Hashim Spunda | CHAUMA | 49,256 | 0.32 |
Janken Kasambala | NRA | 8,028 | 0.05 |
Macmillan Lyimo | TLP | 8,198 | 0.05 |
Fahmi Dovutwa | UPDP | 7,785 | 0.05 |
Akizungumzia
kutoidhinishwa kwa matokeo hayo na wawakilishi wa Chadema, mkurugenzi wa
uchaguzi katika tume Bw Ramadhan Kailima alisema sheria inawaruhusu kuendelea
na kutangaza matokeo hata bila chama chochote kile kuwakilishwa au kuidhinisha
matokeo husika.
Kwenye
uchaguzi huo, kati ya wapiga kura 23,161,440 waliojiandikisha, ni 15,589,639
waliopiga kura, ambao ni asilimia 67.31 ya wapiga kura wote. Kura 402,248
ziliharibika.
Kufuatia
kutangazwa kwa matokeo hayo, tume hiyo ya uchaguzi sasa inatarajiwa kumkabidhi
Bw Magufuli cheti cha kuwa mshindi wa urais.
Muda mfupi
baada ya kutangazwa kwa matokeo, chama hicho kimeanza kusherehekea kwenye
mtandao wa Twitter huku wafuasi wake nao wakianza kusherehekea katika barabara
za miji.
|
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630. |
No comments:
Post a Comment