EPL 2013/2014:-Penati ya dakika ya 76 yaiua Arsenal Britannia Stadium na pigo hili limewaacha wakiwa Pointi 4 nyuma ya Vinara Chelsea. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Sunday, March 02, 2014

demo-image

EPL 2013/2014:-Penati ya dakika ya 76 yaiua Arsenal Britannia Stadium na pigo hili limewaacha wakiwa Pointi 4 nyuma ya Vinara Chelsea.

.com/simgad/
article-2570396-1BF08FC300000578-209_634x461

Shujaa wa Hat-trick: Andre Schurrle akishangilia baada ya kukamilisha mabao matatu ndani ya dakika 16 peke yake na kuiwezesha Chelsea kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza kufuatia ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham jana March 01,2014.
article-2570396-1BF0BCC900000578-84_634x426

Schurrle alifunga mabao hayo dakika za 52, 65 na 69, wakati bao la kufutia machozi la Fulham lilifungwa na Heitinga dakika ya 74 na Chelsea sasa inatimiza pointi 63 baada ya kucheza mechi 28, ikifuatiwa na Liverpool pointi 59 ,sawa na Arsenal pointi 59 mechi 28 wakati Manchester City ni ya nne pointi 57 mechi 26.
article-2570410-1BF09E4200000578-350_634x395

Wachezaji wa Arsenal wakiwa na nyuso za kusikitika baada ya Walters alikwenda kuukwamisha nyavuni mkwaju huo dakika ya 76 baada ya Laurent Koscielny wa Arsenal kuunawa mpira kwenye eneo la hatari.
article-2570410-1BF08F6F00000578-861_634x383

Miguu 12 ya mtu mzima: Walters akimpoteza maboya kipa wa Arsenal Szczesny na kufuta matumaini ya Arsenal kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza yakififia baada ya jana March 01,2014, kuchapwa 1-0 na Stoke City, bao pekee la Jon Walters kwa penalti kipindi cha pili.
article-2570410-1BF0960B00000578-418_634x472

Jonathan Walters akishangilia na Peter Crouch baada ya kufunga penalti iliyoipa Stoke ushindi wa 1-0.

Jana March 01,204,Chelsea ilizidi kupaa kileleni mwa Ligi kuu soka Uingereza baada ya kuifunga Fulham Bao 3-1 huku Bao la Fulham lilifungwa na Johnny Heitinga wakati Arsenal, ambayo iko Nafasi ya Pili nyuma yao, kupigwa Bao 1-0 na Stoke City.

Penati ya dakika ya 76 ya Jonathan Walters iliwapa ushindi Stoke City wa Bao 1-0 walipopambana kwao Britannia Stadium na Arsenal ambao pigo hili limewaacha wakiwa Pointi 4 nyuma ya Vinara Chelsea.

Penati hiyo ilitolewa baada ya Sentahafu Laurent Koscielny kuunawa Mpira.
Kipigo hiki kimeifanya Arsenal iwe imeshinda Mechi 1 tu kati ya 8 zilizopita ndani ya Britannia Stadium na hata ushindi huo Mwaka 2010 haukuleta raha kwani ni Siku hiyo Aaron Ramsey alivunjwa Mguu vibaya.

Pia kipigo hiki kimekuja wakati mbaya kwa Arsenal katika azma yao ya kutwaa Ubingwa Msimu kwa vile Wapinzani wao wanaofuata ni Tottenham, Chelsea na Manchester City ambao watapambana nao ndani ya Wiki mbili. 

_73304920_suar
Luis Suarez.
Wakicheza Uwanja wa Saint Mary, Liverpool wameichapa Southampton Bao 3-0 na kukwea hadi Nafasi ya Pili kutoka Nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu Uingereza.

Bao za Liverpool zilifungwa na Luis Suarez, Dakika ya 16, Raheem Sterling Dakika ya 58 na Penati ya Dakika za Majeruhi ya Steven Gerrard baada ya Suarez kuangushwa na Jose Fonte.

RATIBA/MATOKEO EPL 2013/2014.

Jumamosi Machi 1,2014.

Everton 1 West Ham 0
Fulham 1 Chelsea 3
Hull 1 Newcastle 4
Stoke 1 Arsenal 0
 Southampton 0 v Liverpool 3

RATIBA EPL.
Jumapili Machi 2,2014.

1930 Aston Villa v Norwich
1930 Swansea v Crystal Palace
1930 Tottenham v Cardiff

Position Team Played Goal Difference Points
1 Chelsea 28 30 63
2 Liverpool 28 38 59
3 Arsenal 28 24 59
4 Man City 26 42 57
5 Tottenham 27 3 50
6 Everton 27 11 48
7 Man Utd 27 12 45
8 Newcastle 28 -2 43
9 Southampton 28 3 39
10 West Ham 28 -4 31
11 Hull 28 -5 30
12 Stoke 28 -14 30
13 Swansea 27 -4 28
14 Aston Villa 27 -10 28
15 Norwich 27 -19 28
16 Crystal Palace 26 -18 26
17 West Brom 27 -8 25
18 Sunderland 26 -16 24
19 Cardiff 27 -29 22
20 Fulham 28 -34 21

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *