Picha:- Mwili wa Nelson Mandela’’Madiba's ulivyowasili kijijini Qunu kwa ajili ya Mazishi ya Kimila kwa Ng'ombe dume kuchinjwa (Jumapili Desemba 15). - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, December 14, 2013

Picha:- Mwili wa Nelson Mandela’’Madiba's ulivyowasili kijijini Qunu kwa ajili ya Mazishi ya Kimila kwa Ng'ombe dume kuchinjwa (Jumapili Desemba 15).

Former president Nelson Mandela's body touched down at the Mthatha Airport at 1.37pm on Saturday. He was given full military honours at Mthatha Airport. Picture: eNCA.

Former president Nelson Mandela's body touched down at the Mthatha Airport at 1.37pm on Saturday. Picture: eNCA

Former president Nelson Mandela's body touched down at the Mthatha Airport at 1.37pm on Saturday. He was given full military honours at Mthatha Airport. Picture: eNCA

Former president Nelson Mandela's body touched down at the Mthatha Airport at 1.37pm on Saturday. He was given full military honours at Mthatha Airport. Picture: eNCA

The airforce C-130 Hercules aircraft carrying former president Nelson Mandela's body touched down at the Mthatha Airport at 1.37pm on Saturday. Picture: eNCA

Former president Nelson Mandela's body touched down at the Mthatha Airport at 1.37pm on Saturday. He was given full military honours at Mthatha Airport. Picture: eNCA.
Ng'ombe dume (fahali) atachinjwa kisha kuwekwa katika kaburi atakamozikwa Rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Mzee Nelson Mandela, Kijiji cha Qunu, Mthatha Jimbo la Eastern Cape Jumapili hii(Desemba 15,2013).

Viongozi wa kimila wa Kabila la AbaThembu wametoa mwito kwa Serikali ya Afrika Kusini isiingilie taratibu za mazishi ya kiongozi huyo na kuonya kwamba ikifanya hivyo, 'Mandela hatapokewa na miungu' na kwamba roho yake inaweza kurejea na kuathiri familia.

The motorcade escorting the body
the Nelson Mandela ahead of his State
funeral, passes through Mthatha
enroute to Qunu, where he will be buried. 
"Jumapili baada ya mwili wake kuwekwa katika kaburi lake, taratibu zote za kimila zitafanywa na Himaya ya Kifalme," alisema Kiongozi wa Jamii ya Xhosa, Nokuzola Mndende baada ya kutembelea familia ya Mandela, nyumbani kwao Houghton, Johannesburg na kuongeza:

"Zitakuwa ni mila na desturi za jadi, Serikali inapaswa kutupa nafasi na isituingilie. Fahali (ng'ombe dume) atachinjwa kwa ajili ya kumsindikiza, ni familia ya Mandela pekee watakaohusika na taratibu hizi za kumwandalia safari njema."

Mandela anazaliwa katika Kabila la AbaThembu ambalo linazungumza Ki- Xhosa na kwa mujibu wa taratibu za kabila hilo, hata mwili wake utashushwa kaburini na viongozi wa kimila.

Hata hivyo, habari zaidi kutoka Qunu zinasema licha ya taratibu za kimila, pia kutakuwapo taratibu za Dini ya Kikristo, ambayo Mandela alikuwa muumini wake.

Jumamosi Decemba 14, mwili wa Mandela ulisafrishwa kutoka Uwanja wa Ndege wa Jeshi wa Waterkloof, Pretoria hadi Mthatha, Eastern Cape kwa ajili ya mazishi leo Jumapili.

Viongozi wa juu wa Chama Tawala cha ANC, nao walitoa heshima za mwisho muda mfupi kabla ya mwili huo kusafirishwa.

Taarifa ya Idara ya Habari na Mawasiliano ya Afrika Kusini (GICS), ilisema Jeshi la Afrika Kusini (SANDF), ndilo litakaloongoza shughuli zote za kuagwa kwa mwili wa Mandela.

Mazishi rasmi ya jumapili yatahudhuriwa na watu kama elfu tano hivi wakiwemo pia viongozi mashuhuri wa kimataifa ikiwa ni pamoja na mwanamfalme Charles wa Uingereza.

"Kamera hazitaruhusiwa wakati wa mazishi, familia haitaki watu waone maiti itakapoteremshwa kaburini," amesema msemaji wa serikali Phumla William.

Vyombo vya habari na wageni wa hishma hawatoweza kuhudhuria, amesisitiza.

Hitimisho la siku 10 za maombolezo ya msiba wa Mandela itakuwa Jumapili, Desemba 15 wakati kiongozi huyo atakapozikwa katika makaburi ya familia.

Wakati wa mazishi SANDF pia wamepewa jukumu la kusimamia upelekaji jeneza makaburini na heshima za kitaifa zitatolea pamoja na wimbo wa Taifa kupigwa kabla ya maziko.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad