![]() |
Theo Walcott
alirejea uwanjani kwa mara ya kwanza leo tangu Septemba na akafunga mabao
mawili ya Arsenal dakika za 31 na 63, wakati lingine lilifungwa na beki Per
Mertesacker dakika ya 90.
|
![]() |
Mabao ya Manchester
City yamefungwa na Sergio Aguero dakika
ya 14, Alvaro Negredo dakika ya 39 Fernandinho mawili dakika za 50 na 88 David
Silva dakika ya 66 na Yaya Toure dakika ya 90.
|
Vinara wa
Ligi Kuu Uingereza, Arsenal leo (Desemba 14,2013) huko Jijini Manchester
Uwanjani Etihad wamebamizwa na Manchester
City Bao 6-3 katika Mechi ambayo City waliitawala kabisa.
Kipigo hiki
kimefanya uongozi wa Arsenal upunguzwe uwe Pointi 3 tu na Man City kukamata Nafasi ya tatu huku Chelsea wakaweza kuwapiku baada ya kuifunga
Crystal Palace bao 2-1 na kufanya pengo lao na Arsenal kuwa Pointi 2 tu.
Hiki ni
kipigo cha 3 kwa Arsenal katika Ligi baada kufungwa 3-1 na Aston Villa ndani ya
Emirates katika Siku ya Ufunguzi wa Msimu na kisha kuchapwa 1-0 na Mabingwa Man
United Uwanjani Old Trafford.
Nyota wa
Mechi hii ni Mbrazil Fernandinho ambae alinyakuwa Tuzo ya Mchezaji Bora wa
Mechi na pia kupiga Bao 2.
Man City
wameendeleza wimbi lao la kumimina mvua za Magoli Uwanjani kwao Etihad na sasa
imepiga Bao 22 katika Mechi zao 4 zilizopita kwa kuichapa Swansea City 3-0,
kuifumua Tottenham 6-0, kuirarua Norwich City 7-0 na leo kuwabomoa Arsenal Bao
6-3.
Latest Football
- Man City 6 - 3 Arsenal FT
- Cardiff 1 - 0 West Brom FT
- Chelsea 2 - 1 Crystal Palace FT
- Everton 4 - 1 Fulham FT
- Newcastle 1 - 1 Southampton FT
- West Ham 0 - 0 Sunderland FT
Mechi
inayofuata kwa Arsenal kwenye Ligi ni Nyumbani kwao Emirates watakapopambana na
Chelsea hapo Desemba 23.
As It Stands Table
Position | Team | Played | Goal Difference | Points |
---|---|---|---|---|
1 | Arsenal | 16 | 16 | 35 |
2 | Chelsea | 16 | 14 | 33 |
3 | Man City | 16 | 29 | 32 |
4 | Everton | 16 | 12 | 31 |
5 | Liverpool | 15 | 16 | 30 |
6 | Newcastle | 16 | -1 | 27 |
7 | Tottenham | 15 | -1 | 27 |
8 | Southampton | 16 | 5 | 24 |
9 | Man Utd | 15 | 3 | 22 |
10 | Swansea | 15 | 1 | 19 |
11 | Aston Villa | 15 | -2 | 19 |
12 | Hull | 16 | -6 | 19 |
13 | Stoke | 16 | -5 | 18 |
14 | Cardiff | 16 | -10 | 17 |
15 | Norwich | 15 | -14 | 17 |
16 | West Brom | 16 | -5 | 15 |
17 | West Ham | 16 | -6 | 14 |
18 | Crystal Palace | 16 | -13 | 13 |
19 | Fulham | 16 | -15 | 13 |
20 | Sunderland | 16 | -18 | 9 |
RATIBA
[Saa za
Bongo]
Jumapili
Desemba 15,2013.
16:30 Aston
Villa v Man United
16:30
Norwich v Swansea
19:00
Tottenham v Liverpool
nice information kipigo-cha
ReplyDelete