Umeuona
mlango? Mwang'oka akishuka garini wakati wa Maonesho ya 37 ya Sabasaba yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam mwaka huu 2013).
|
Mwangoka anasema kwa juu kuna roof ya kupitisha upepo.
|
Kwa ndani ……Umeona dashboard yake ilivyo ambapo robu tatu ya vitu
vilivyotengeneza ni mbao.
|
Mbunifu Kenneth Joseph Mwang'oka akiwa katika pozi ndani ya gari lake hilo likiwa katika viwanja vya Maonesho ya 37 ya Sabasaba
yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam mwaka huu 2013.
|
Gari hilo linaloonekana kwa mbele ambapo robu tatu ya vitu
vilivyotengeneza ni mbao.
|
Watu wakilishangaa gaari hilo Mbunifu gari hilo likiwa katika viwanja vya Maonesho ya 37 ya Sabasaba hivi karibuni
jijini Dar es Salaam mwaka huu 2013.
|
Umeona vitendea kazi vyake vilivyo na inatumia mafuta lita moja kwa
kilomita nane.
|
|
Muonekano wa
gari hilo kwa nyuma likiwa katika
viwanja vya Maonesho ya 37 ya Sabasaba hivi karibuni jijini Dar es Salaam mwaka huu 2013.
|
Keneth Mwang'oka akiwa ndani ya gari lake ,Gari ya mbao iliyobuniwa na mkazi huyo
wa kijiji cha Nyololo mkaoni Iringa anasema hata rivasi kama kawa unaliendesha tu.
|
Ama kweli TANZANIA
imejaliwa watu wenye vipaji na ujuzi
mkubwa katika nyanja ya Sayansi na Teknolojia ila kuna vitu vidogo
vinavyowakwaza kusimama na kwenda sambamba na wataalam wa mataifa mengine ambao
wapo mbali katika suala la vipaji na ubunifu.
Mifano michache ni watu wanaomudu kutengeneza magobole, mashine mbalimbali na vitu vingine na hata wabunifu wa mrusho wa matangazo ya radio, ambao badala ya kuwezeshwa hupata vikwazo ikiwamo kunaswa na vyombo vya dola na kufunguliwa mashtaka ilihali wangeweza kutumika kuitangaza Tanzania.
Hapo juu ni mmoja wa wabunifu wa Kitanzania aliyeweza kutengeneza gari ambalo alitumia muda wa miezi sita kulikamilisha kwa kuokoteza vifaa na kulipamba kiasilia kwa kutumia malighafi ya misitu.
Majina yake kamili ni Kenneth Joseph Mwang'oka ambaye alikuwa moja ya vivutio katika Maonyesho ya Biashara ya Sabasaba kwa ubunifu wa gari hilo linalotumia injini ya Toyota na kuongeza ubunifu wao kiasi kwamba gari hilo lililomgharimu kiasi cha Sh Milioni 8.6 kutembea kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Mwenyeji huyo wa mkoa wa Mbeya, lakini ubunifu wake kaufanyia mjini Iringa anasema lengo lake ni kuhakikisha anakuja kutengeneza vitu zaidi ya gari hilo la aina yake.
No comments:
Post a Comment