CHADEMA. |
Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema), `kimefunika' katika uchaguzi mdogo wa
madiwani uliofanyika kwenye kata nne za Jimbo la Arusha Mjini uliofanyika jana(Julai 14,2013).
Matokeo
katika vituo mbalimbali vya kata hizo nne ambayo kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), yalionyesha
Chadema ikiongoza kwa idadi kubwa ya kura zilizopigwa kwenye vituo 136 vya
kupigia kura huku kikifuatiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Matokeo
kamili katika vituo hivyo yalikuwa kama ifuatavyo:-
Katika
Kata ya Elerai, mgombea wa CHADEMA Injinia Jeremia Mpinga alimbwaga Emanueli
Laizer wa CCM kwa kura 1,715, dhidi ya 1,239.
Kata
hiyo ilikuwa na wapiga kura 23,797 waliojiandikisha na vituo 55 vya kupigia kura,
lakini idadi kubwa ya wananchi hawakujitokeza.
Matokeo
ya kura yalitangazwa chini ya ulinzi mkali wa askari polisi zaidi ya 40 wenye
silaha, na kupokelewa kwa shangwe kubwa na wafuasi na mashabiki wa CHADEMA.
Katika
Kata ya Kaloleni, mgombea wa CHADEMA, Kessy Emmanuel Miliare alimshinda kwa
mbali mgombea wa CCM kwa kura 1,470 dhidi ya 530, wakati mgombea wa CUF
ameambulia kura 275. waliojiandikisha 12,674 waliopiga kura 2,292. Kura halali
ni 2,277 na zilizoharibika 15.
Akitangaza
matokeo katika Kata ya Themi, Msimamizi wa Uchaguzi, Editha Mboye alimtangaza
mgombea udiwani wa CHADEMA, Mallance Kinabo kuwa mshindi kwa kupata kura 678,
akimwacha mbali mgombea wa CCM Victor Mkolwe aliyepata kura 326, huku yule wa
CUF, Lebora Ndervai akipata kura 313.
Wafuasi wa CHADEMA. |
Kata
ya Kimandolu, CHADEMA pia wameibuka na ushindi mkubwa na kuiacha vibaya CCM.
Mgombea
wa CHADEMA, Elishadai Ngowi amemshinda mgombea wa CCM, Edina Sauli kwa kura
2,265, dhidi ya 1,169 za mpinzani wake.
Mara
baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Jiji la Arusha lilizizima kwa shangwe na
nderemo, huku idadi kubwa ya watu wakijipongeza kwa ushindi huo mkubwa.
No comments:
Post a Comment