Mkoa
wa Kagera,unakabiliwa na wimbi la wahamiaji haramu wanaokadiriwa kufikia 32,000
ambao huingia njia za panya.
Naibu
Kamishina wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kagera George Kombe aliiambia MTANZANIA
mjini Bukoba jana(Julai 13,2013).
Alisema
wahamiaji hao, wanaingia mkoani Kagera kupitia maeneo ya Murongo, Kanyigo,
Rusumo, Mtukura, Bugango na Kabanga mkoani Humo.
Alisema
kutokana na kuwepo kwa wahamiaji hao, idara yake inakadiria kutumia Shilingi Milioni
650, kwa ajili ya kufanya operesheni ya kuwarudisha makwao.
Alisema
wahamiaji wengi, wanatoka nchi za Rwanda, Burundi, Uganda na Jamhuri ya
Kidemokrasi ya Kongo (DRC).
Alisema
pamoja na idadi hiyo, bado wanaendelea na kazi ya kuwatambua wahamiaji wengine.
Alisema,
pamoja na jitihada hizo, bado kuna baadhi ya viongozi wakiwamo wenyeviti wa
vitongoji ambao wanawahifadhi majumbani mwao.
Alisema
mwaka 2006, walifanya operesheni kama hiyo ambapo walitumia Sh milionin 450.
No comments:
Post a Comment