Msajili wa vyama vya
siasa nchini Tanzania ,Bw. John Tendwa.
|
Hatimaye
msajili wa vyama vya siasa nchini, John Tendwa ameibuka na kusema sasa anaandaa
kalamu yake kukifuta Chama kikuu cha upinzani nchini CHADEMA.
CHADEMA. |
Katika
Taarifa yake kwa vyombo vya habari muda mfupi uliopita Tendwa amesema CHADEMA
wanataka kuanzisha kikundi cha mgambo ambacho ni kinyume na sheria, katiba ya
nchi na sheria za usajili wa vyama.
Msajili
huyo amesema kwamba kama madai ya CHADEMA ni kuanzisha kikundi cha kujilinda
dhidi ya Green Guard wa CCM madai hayo hayana msingi wowote kwani kama CHADEMA
wana taarifa kwamba Green Guard wanahatarisha amani basi wanapaswa kuripoti
suala hilo Polisi ili lifanyiwe kazi kwa mujibu wa sheria.
Tendwa
amezidi kuonya kwamba uamuzi wake ni wa mwisho na atakapoifuta CHADEMA maamuzi
yake hayapingwi popote kisheria.
Source:
JF
No comments:
Post a Comment