Wananchi wa Kijiji cha Rulenge Wilayani Ngara Mkoani Kagera wamlalamikia Bw.Pius Ngeze kuwapora Ardhi . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, July 14, 2013

Wananchi wa Kijiji cha Rulenge Wilayani Ngara Mkoani Kagera wamlalamikia Bw.Pius Ngeze kuwapora Ardhi .


Picha Juu na Chini ni Wananchi wa kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera   wakiwa katika Mkutano wa hadhara katika ofisi za Tarafa ya Rulenge walipokutana hivi karibuni kumtaka mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoani Kagera Bw Pius Ngeze kuachia sehemu ya ardhi anayomiliki kijijini humo kwa kuwa aliipata kinyume na utaratibu.




Wananchi wa kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera   wakiwa katika Mkutano wa hadhara katika ofisi za Tarafa ya Rulenge walipokutana hivi karibuni kumtaka mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoani Kagera Bw Pius Ngeze kuachia sehemu ya ardhi anayomiliki kijijini humo kwa kuwa aliipata kinyume na utaratibu.



Kutoka kushoto ni Mbunge wa jimbo la Ngara Bw.Deogratius Ntukamazina na Mkuu wa Wilaya ya Ngara Bw.Kostantine Kanyasu wakiwa katika Mkutano huo wa Wananchi wa kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera   walipokutana hivi karibuni kumtaka mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoani Kagera Bw Pius Ngeze kuachia sehemu ya ardhi anayomiliki kijijini humo kwa kuwa aliipata kinyume na utaratibu.


Bw Pius Ngeze akijibu hoja mbalimbali za Wananchi hao na kusema kuwa  alipata ardhi hiyo ikiwa ni pori lisilokuwa na watu yeye na ndugu zake tisa waliokuwa na familia ya watu 30 mwaka 1983 na walianza kuishi katika eneo hilo mwaka 1984 baada ya kupata barua ya kukubaliwa kupewa ardhi hiyo na katibu wa CCM  wa Tawi la Rulenge(Jina la katibu huyo halikujulikana).


Ndugu yake Ngeze mwl Damiani Ngeze ambaye ndiye mwanzilishi wa kuishi eneo la Mugunzu kijijini humo akitoa ushuhuda katika mkutano huo na kukana kuwa ardhi hiyo haikutolewa kwa utaratibu.


Mwenye sweta la njano ni aliyekuwa mwenyekiti wa kijiji cha Rulenge kati ya mwaka 1977 hadi 1988 Bw Michael Rudigaje akiwa katika mkutano huo na kusema kwamba ardhi hiyo haikutolewa kwa utaratibu .




Mbunge wa Jimbo la Ngara mkoani Kagera Bw.Deogratius Ntukamazina akiongea wakati wa mkutano huo wa Wananchi wa kijiji cha Rulenge  katika ofisi za Tarafa ya Rulenge walipokutana hivi karibuni kumtaka mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoani Kagera Bw Pius Ngeze kuachia sehemu ya ardhi anayomiliki kijijini humo kwa kuwa aliipata kinyume na utaratibu.


Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw Costantine Kanyasu akisisitiza jambo katika mkutano huo na kuagiza uongozi wa kijiji hicho kwa kushirikiana na mwanasheria wa halmashauri ya wilaya Ngara  kuomba  ardhi  hiyo kwa Bw Ngeze kuliko kutumia  nguvu.




Wananchi wa kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera   wakiwa katika Mkutano wa hadhara katika ofisi za Tarafa ya Rulenge walipokutana hivi karibuni kumtaka mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoani Kagera Bw Pius Ngeze kuachia sehemu ya ardhi anayomiliki kijijini humo kwa kuwa aliipata kinyume na utaratibu.


Wananchi wa kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera  wamemtaka mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoani Kagera Bw Pius Ngeze kuachia sehemu ya ardhi anayomiliki kijijini humo kwa kuwa aliipata kinyume na utaratibu.



Wakiongea  (Julai 10,2013 ) katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Wajumbe wa Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya pamoja na Mbunge wa Jimbo la Ngara Bw.Deogratias Ntukamazina ,Wananchi hao walisema wanataka ardhi hiyo kujenga shule ya msingi na kupata sehemu ya makaburi.



Mmoja wa wananchi hao ambaye ni mjumbe wa serikali ya kijiji  Bw Said Biveve alisema wananchi wanahitaji ardhi kwa ajili miradi ya maendeleo na kwamba ardhi hiyo ilipatikana  kwa Ngeze kutumia madaraka kinyume cha sheria akiwa mwenyekiti wa CCM mkoani Kagera.



Naye Martin Mwampamba alisema kuwa kinachohitajika ni Maendeleo wala jamii ya Warulenge haihitaji ruzuku ya serikali katika kujenga shule  ya msingi ambapo katika shule mama ya Rulenge ina msongamano wa wanafunzi wapatao 1437 na kukosa vyumba vya madarasa .



Akijibu hoja za Wananchi hao Bw Pius Ngeze alisema kuwa alipata ardhi hiyo ikiwa ni pori lisilokuwa na watu ,yeye na ndugu zake tisa waliokuwa na familia ya watu 30 mwaka 1983 na walianza kuishi katika eneo hilo mwaka 1984 baada ya kupata barua ya kukubaliwa kupewa ardhi hiyo na katibu wa CCM  wa Tawi la Rulenge(Jina la katibu huyo halikujulikana).



Bw.Ngeze alidai kuwa tangu aishi pale akitokea kijiji na kata ya Muganza iliyopo mpakani na nchi Jirani ya Burundi  baada ya majambazi kumuua baba yake na kwamba mgogoro huo wa kudai ardhi umeibuka tangu mwaka 2010 ambapo alifikisha kesi katika Mahakama ya ardhi ya Chato na kupata ushindi juu ya ardhi hiyo.



Kwa mujibu wa barua ya kupewa ardhi kama kielelezo cha hati ya Mahakama inaonesha kuwa ardhi hiyo ambayo haioneshi ni ekari kiasi gani ni mali yake na ndugu zake japo baadhi yao katika mkutano huo walimkana kwamba anatumia mabavu  katika kuimiliki.



Hata hivyo aliyekuwa mwenyekiti wa kijiji cha Rulenge kati ya mwaka 1977 hadi 1988 Bw Michael Rudigaje  na ndugu yake Ngeze Mwl. Damiani Ngeze ambaye ndiye mwanzilishi wa kuishi eneo la Mugunzu kijijini humo wamekana kuwa ardhi hiyo haikutolewa kwa utaratibu.



Kwa upande wake  Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw Costantine Kanyasu ameagiza uongozi wa kijiji hicho kwa kushirikiana na mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya Ngara kuomba  ardhi kwa Bw Ngeze kuliko kutumia  nguvu kwani ardhi hiyo inamilikiwa kihalali kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1999 iliyoanza kutumika mwaka 2002. 



Aidha Bw kanyasu amesema mlalamikiwa licha ya Mahakama kumpatia  uhalali wa kumiliki  ardhi hiyo hana budi kutumia busara kuwakubalia wananchi kujenga shule na kupata sehemu ya makaburi ili wajenge mahusiano mema na jamii inayomzunguka kuliko kuwa na migogoro. 


 Habari Na :Shaaban Ndyamukama.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad