Miili ya Wanajeshi wa Tanzania waliofia Sudan yawasili Tanzania na itaagwa kwa heshima zote siku ya Jumatatu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, July 21, 2013

Miili ya Wanajeshi wa Tanzania waliofia Sudan yawasili Tanzania na itaagwa kwa heshima zote siku ya Jumatatu.


Baadhi ya wanajeshi na wahudumu wa ndege wakishusha miili ya wanajeshi wa JWTZ walinda amani saba raia wa Tanzania waliuawa na wengine kumi na saba kujeruhiwa baada ya shambulizi kutekelezwa na kundi ambalo halijafahamika huko Darfur mnamo tarehe 13 mwezi Julai,Mwaka huu.




Baadhi ya askari wa JWTZ wakifunika majeneza ya askari hao kwa bendera ya taifa la Tanzania mara baada ya kuwasili jana(Julai 20,2013)  katika uwanja wa  kimataifa  wa mwalimu Julias  Kambarage Nyerere wakati ndege yenye  namba  B 737-400 iliyobeba miili ya wanajeshi  hao wa Tanzania waliopoteza maisha  nchini  sudan ilipokuwa ikikanyaga katika ardhi ya tanzania tayari  kupokelewa na ndugu jamaa na marafiki.




Makamu wa Rais wa Tanzania  Dk Gharib Bilal akiongoza viongozi mbalimbali na maofisa wa jeshi la JWTZ, Jeshi la Polisi na wengine mbalimbali kupokea miili hiyo hapo Jana(Julai 20,2013).


Baadhi ya askari wa JWTZ wakibeba miili ya wanajeshi wenzao waliouwawa Darfur kuiingiza kwenye magari maalum kabla ya kuondolewa katika uwanja wa jeshi,aidha wanajeshi hao walinda amani saba raia wa Tanzania waliuawa na wengine kumi na saba kujeruhiwa baada ya shambulizi kutekelezwa na kundi ambalo halijafahamika huko Darfur mnamo tarehe 13 mwezi Julai,2013.



Baadhi ya askari wa JWTZ wakibeba miili ya wanajeshi wenzao waliouwawa Darfur kuiingiza kwenye magari maalum kabla ya kuondolewa katika uwanja wa jeshi.


Baadhi ya askari wa JWTZ wakibeba miili ya wanajeshi wenzao waliouwawa Darfur kuiingiza kwenye magari maalum kabla ya kuondolewa katika uwanja wa jeshi,aidha wanajeshi hao walinda amani saba raia wa Tanzania waliuawa na wengine kumi na saba kujeruhiwa baada ya shambulizi kutekelezwa na kundi ambalo halijafahamika huko Darfur mnamo tarehe 13 mwezi Julai,2013.



Miili ya wanajeshi saba wa Tanzania waliokuwa katika kazi za kutekeleza ulinzi wa amani wa kimataifa katika mkoa wa Darfur nchini Sudan imewasili Jumamosi  na ndege maalumu ya Umoja wa Mataifa.


Wanajeshi hao waliuwawa  mwezi Julai, kufuatia shambulizi la ghafla wakiwa nchini Sudan.


Kaimu mkurugenzi wa habari wa JWTZ, Meja Joseph Masanja anasema miili hiyo imewasili  Jumamosi majira ya saa kumi kasorobo katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu J. K. Nyerere na imehifadhiwa katika hospitali ya jeshi ya Lugalo hadi Julai 22 ambapo itaagwa rasmi.



Miili ya wanajeshi hao saba iliyowasili jana (Julai 20,2013) ni SajIni Shaibu Sheha Othman, Koplo Osward Paulo Chaula, Koplo Mohamed Juma Ally, Koplo Mohamed Chukilizo, Private Rodney Ndunguru, Private Peter Werema na Private Fortunatus Msofe.



Wanajeshi hao walikuwa sehemu ya Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa (Unamid), kusini mwa Darfur na walitoka katika vikosi vya, 42KJ Chabruma, Songea, 44KJ Mbeya, 36KJ Msangani, 92KJ Ngerengere, 94KJ cha Mwenge, Dar es Salaam, 41KJ Nachingwea na Makao Makuu ya JWTZ- Upanga, Dar es Salaam.



Wakati taratibu za maziko zikiandaliwa mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC Fatou Bensuda ametoa onyo kali kuhusu shambulizi la hivi karibuni lililowalenga waangalizi wa amani kutoka umoja wa mataifa na jeshi la umoja wa afrika huko Darfur sudan na kusema kuwa linaweza kuhesabika kama uhalifu wa kivita.



Katika taarifa yake akiwa Heague Fatou Bensuda amekumbusha pande zote zenye mgogoro kufahamu kuwa mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ina mamlaka jimboni Darfur.



Rais Kikwete.
Aidha  RAIS wa Tanzania  Jakaya Mrisho Kikwete amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na Rais wa Sudan Omar Bashir kufuatia kuuawa na kujeruhiwa kwa askari wa Tanzania, walioko katika ulinzi wa kimataifa wa amani katika jimbo la Darfur na kumtaka Rais Bashir kuchukua hatua za haraka kuwasaka na kuwakamata waliohusika na kitendo hicho kiovu na kuwafikisha  mbele ya sheria haraka iwezekanavyo. 



Katika mazungumzo yao, Rais Omar Bashir amekubaliana na Rais Kikwete na kumuahidi kuwasaka hadi kuwakamata wale wote waliohusika na kuwachukulia hatua za kisheria.


Rais Bashir amemueleza Rais Kikwete kuwa binafsi anaamini kuwa waliohusika ni wahalifu na hivyo kuahidi kuwa lazima watasakwa hadi kukamatwa kwa ajili ya kuchukuliwa hatua. 


Rais Bashir amempa pole Rais Kikwete kwa tukio hilo la kusikitisha ambapo wanajeshi wa Tanzania wameenda nchini Sudan kulinda Amani na Usalama wa wananchi wa Sudan.

Mapema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Bw. Ban Ki Moon alimpigia Rais Kikwete na kumpa pole kwa mkasa huo mkubwa na wa kusikitisha ambao umewatokea wa Tanzania hao wakati wakiwa katika kutekeleza jukumu lao la kulinda amani nchini Sudan.


Hadi sasa hakuna kikundi chochote ambacho kimekiri kuhusika na shambulio hilo ingawaje kumekua na kutupiana lawama baina ya vikundi vya kiserikali na vya waasi katika jimbo la Darfur.


Mapigano baina ya vikundi vya kikabila na koo mbalimbali zimesababisha mapigano na uvunjifu mkubwa wa amani na usalama katika jimbo la Darfur kwa muda wa miaka 10 sasa, na mara nyingi mapigano na tofauti zao hizo zimesababisha vifo na uvunjifu wa amani kwa wananchi wa Sudan na wageni pia.

Mwishoni mwa mwaka jana Wanajeshi wanne kutoka Nigeria waliuawa karibu na El Geneina , Magharibi mwa Darfur ambapo pia inaelezwa na Umoja wa Mataifa kuwa wanajeshi wapatao 50 wameuawa tangu kikosi hiki cha Umoja wa Afrika kinachoundwa kwa pamoja chini ya Umoja wa Mataifa (UNAMID) kianze operesheni yake mwishoni mwa mwaka 2007.

Taarifa za Umoja wa Mataifa pia zinaeleza kuwa kabla ya mashambulizi yaliyofanyika dhidi ya kikosi cha Tanzania jumamosi iliyopita, wanajeshi 6 wanaolinda Amani wameuawa tangu oktoba mwaka Jana huu ambapo pia inasadikiwa kuwa watu wapatao 300,000 wameyakimbia makazi yao.

Hata hivyo kiini cha mgogoro huo unaosadikiwa kuwa ni ugomvi wa ardhi na rasilimali zilizoko katika jimbo hilo nchini Sudan.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad