Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP
Said Mwema.
|
Na
Shaaban Ndyamukama BIHARAMULO:
Kundi
la watu wapatao 15 wanaosadikiwa kuwa majambazi limeteka mabasi mawili ya
abiria yanayosafiri kutoka Bukoba kuelekea Dare es Salaam na kupora mali mbali
mbali za abiria katika wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera.
Kamanda
wa jeshi la polisi mkoani kagera Bw Philipo Karangi amesema tukio hilo
limetokea leo July 15, 2013 saa mbili asubuhi kwenye eneo la mlima wa simba ulioko katikati ya pori la hifadhi ya Biharamulo na kujeruhi
abiria baada ya kupiga risasi kadhaa kwenye
magari hayo.
Bw
Karangi ametaja magari yaliyotekwa kuwa ni RS lenye namba za usajili T. 495 ATG
na NBS lenye namba za usajili T 644 BUR na kwamba abiria 13 wamejeruhiwa
lakini 12 wamepata matibabu katika
Hospitali teule ya ya Biharamulo kisha kuendelea na safari zao.
Amesema
kuwa majambazi hao walikuwa na silaha aina ya SMG sita na LMG mbili na katika
kuteka magari hayo waliweza kupora silaha aina ya SMG aliyokuwa nayo askari polisi aliyekuwa amesindikiza moja ya
mabasi hayo na kuondoka nayo porini.
Kwa
upande wake Mganga mkuu wa haospitali ya Biharamulo Bw Grasmus Sebuyoya amesema
majeruhi mmoja Fedrick Rugaihula mkazi wa Bukoba ndiye hali yake sio nzuri
baada ya kupigwa risasi kichwani jirani
na shingo na amelwazwa katika hospitali hiyo kwa matibabu zaidi.
Akiongea
na mwanahabari hizi kwa njia ya simu kondakta wa basi la NBS Amiri Omari akiwa
amefika eneo la Runzewe akielekea Arusha
amesema kuwa majambazi hao lengo lao ilikuwa ni kupata fedha na simu za
mkononi.
“Kusema
kweli ndugu yangu hali ilikuwa sio kwani walipiga risasi kioo cha mbele ya
dreva na abiria mmoja kupatwa jirani na shingo na kuanza kuvuja huku wengine
wakichanwa na vipande vya vioo na hapo kusakwa kutaka kuwasilisha fedha”alisema
Omari.
Amesema
kuwa katika tukio hilo kulikuwa na maroli mawili yaliyokuwa yamesimamishwa na
mabasi hayo katika kusimama kujua nini kinaendelea kulitokea purukushani za
risasi na abiria kuanza kuporwa mali zao kwenye pori la barabara itokayo Muleba
kuingia mjini Biharamulo .
Hata
hivyo kamanda karangi amesema kuwa jeshi
la polisi wilayani Biharamulo linaendelea kusaka majambazi hayo katika pori
hilo kwa kushirikiana na askari wa wanyamapori katika hifadhi ya wanyama ya
Biharamulo ili kuwatiambaroni ili kufikishwa katika mkondo wa sheria .
Matukio
ya ujambazi wilayani Biharamulo yamekuwa yakitokea mara kwa mara katika hifadhi hiyo ambapo
changamoto kubwa ni kwa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ambayo kwa sasa majeshi yake yako
katika mazoezi ya sherehe za mashujaa zinazotarajia kufanyika Julai 25 mkoani
kagera.
No comments:
Post a Comment