*Dunia
nzima inaadhimisha siku ya Mzee Nelson. Mandela hivi leo...*Binafsi
Najifunza Mengi sana toka kwa Kiongozi huyu Mzalendo toka Africa ya
Kusini..*MAARIFA..*..BIDII..*..JUHUDI..*UKARIMU..*..HEKIMA..*..UPENDO..*..Lakini
pia tujue kuwa ..*MARADHI. humpata mtu Na..*UMRI..*WAKATI..na
..*MAUTI..havimsubiri mtu...Happy Birthday Mzee Madiba..Mola akupe
taafifu na heri pia..**
Like · · Unfollow Post · Share
- Majaliwa Ngonyani, Mwalimu Kaijage, Shama Getruda and 10 others like this.
- Awami Hassan 2namtakia kila la kher happy birthday mzee madiba
- Elipendo Christopher happy bday baba
- Shimi Mahuba DA UMENIKUMBUSHA SANA NIMEMIC KWAITO ZA KUSINI MWA AFRIKA ILA HAPPYBATHDAY MADIBA NTAENJOY KUCHEZA KWAITO TU PAMOJA MZAZ
- Mohamed Makonda Mengi sana kila mtu nayakumbuka toka 1994 hadi 1999. wakati wa utawala wake wa Urais....Leo Mzee Mgonjwa ..umri wake umeenda Basi Sala na Maombi pia tuzidi kumuombea
- Potentine Kagombora Du!asante kwa kutukumbusha kaka 2muombee angalau afkishe miaka100 vlevle 2jitahd kufuata nyayo zake.
- Mohamed Makonda @Pote ni kweli Ndugu...** Mzee
Mandela...Leo ametimiza miaka 95 ya kuzaliwa mbali na afya yake kuwa mbaya baada ya kuwa mahututi
kwa muda mrefu katika hospitali moja nchini Afrika Kusini. Tuungane kumtakia kila la kheri Mzee Mandela
katika siku yake ya kuzaliwa leo...**
Rais
wa zamani Mweusi wa Afrika Kusini Mzee
Nelson Mandela ametimiza miaka 95 leo(Julai 18,2013), akiwa amelazwa
hospitalini kwa muda wa wiki sita.
Ikulu
ya nchi hiyo imetangaza kuwa hali ya mkongwe huyo inaonyesha kuboreka kidogo.
Salamu
zimemiminika leo kumpongeza Mzee Nelson Mandela na kumtakia nafuu ya haraka.
Rais
Barack Obama wa Marekani amesema katika salamu zake kwamba yeye na familia yake
walitiwa hamasa na ushujaa wa Mandela, baada ya kutembelea gereza alikofungiwa
kwa miaka mingi wakati wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi.
Mapema
leo Ikulu ya Afrika Kusini imetoa tangazo linaloarifu juu ya afya ya mzee
Mandela. ''Madiba anabakia hospitalini mjini Pretoria, lakini madaktari
wanaomtibu wanathibitisha kuwa hali yake inaboreka taratibu'', lilisema tangazo
hilo, likitumia jina la kiukoo la Mandela..Madiba.
Hongera Mandela ,kutimiza miaka 95. |
Mbali
na kumpongeza Mandela kwa kutimiza miaka 95, Rais Obama ametoa wito kwa watu
kuadhimisha siku ya Mandela wafanya kazi za kujitolea kwa kuenzi jina lake.
Rais
wa Afrika Kusini Jacob Zuma amewataka watu kuiga mchango wa Mandela na
kujitolea kwake, kwa kuongeza juhudi za kuiendeleza jamii yao. Zuma mwenyewe
atawakilisha mtazamo wa Mandela wa kuzileta pamoja jamii, kwa kuwapa nyumba
watu masikini weupe.
Katika
juhudi hizo, waendesha baskeli watafanya usafi mitaani, wafanyakazi wa
kujitolea watapaka shule rangi, na wanasiasa watashiriki katika miradi mingine
ya kujitolea kwa muda wa dakika 67, kutambua miaka 67 ambayo Mandela amekuwa
mtumishi wa umma. Aidha, wanafunzi wataanza siku yao shuleni kwa kuimba wimbo
'' Happy Birthday Mandela'' wakimtakia heri na kumpongeza kwa kutimiza umri huo
wa miaka 95.
Shughuli
nyingine itakayofanyika kuadhimisha miaka 95 ya Nelson Mandela, ni kumkabidhi
mkongwe huyo kitambulisho kipya cha kisasa, ambacho kitapokelewa kwa niaba yake
na bintiye Zindzi.
Tukio
hilo litakuwa na viashiria mbali mbali kama kumbu kumbu ya enzi za ubaguzi wa
rangi, ambapo raia weusi walilazimishwa kubeba vitambulisho, na hawakuruhusiwa
kutembea katika baadhi ya maeneo, kwa baadhi ya nyakati.
Mwaka
2010, Umoja wa Mataifa uliitangaza tarehe 18 Julai kuwa siku ya Mandela, ambaye
pia ni mshindi wa tuzo ya Nobel ya Amani, lakini mwaka huu, siku hii imekuwa na
umuhimu mkubwa zaidi.
Mandela
amalazwa hospitalini kwa siku 41 sasa akiugua maambukizi ya mapafu, na kwa muda
mrefu hali yake imetajwa kuwa mbaya, lakini ambayo imedhibitiwa na madaktari.
Watu
wa familia yake wamesema kuwa hali hiyo imeimarika kwa kiasi fulani, na anaweza
kupumua kwa msaada wa mashine. Binti yake Zindzi jana aliliambia shirika la
habari la Sky News kwamba kuna wakati walipokuwa wamekata tamaa wakijiweka
tayari kupokea habari mbaya, na kuongeza kuwa kwa sasa anawapa matumaini.
Watu
mbali mbali mashuhuri na wa kawaida wameahidi kujiunga na wananchi wa Afrika
Kusini leo, kumuunga mkono Mzee Mandela katika siku kuu yake ya kuzaliwa.
No comments:
Post a Comment